Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Joseph Kabila ametangaza
baraza la mawaziri la mpito, akikaidi matakwa ya wapinzani wanaomtuhumu
kwa kukiuka makubaliano ya awali.
Kabila ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2001, mwishoni mwa mwaka jana alifikia makubaliano na upinzani kuhusu kuendelea kwake kubaki madarakani baada ya muhula wake wa mwisho kumalizika, lakini makubaliano yao yalivunjika mwezi Machi mwaka huu.
Rais Joseph Kabila
Orodha ya watu 60 waliotangazwa katika nafasi za mawaziri na manaibu waziri inajumuisha majina mengi yaliyokuwa katika mabaraza yaliyotangulia, na wizara muhimu kama ya mambo ya nje, mambo ya ndani, sheria na migodi zimekwenda kwa wapambe wa Rais Kabila.
Baraza jipya litakabiliwa na changamoto kubwa, zikiwemo kuporomoka kwa thamani ya sarafu ya Faranga, na uhaba wa raslimali inayohitajika kuandaa uchaguzi mkuu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.
CHANZO: DW
Kabila ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2001, mwishoni mwa mwaka jana alifikia makubaliano na upinzani kuhusu kuendelea kwake kubaki madarakani baada ya muhula wake wa mwisho kumalizika, lakini makubaliano yao yalivunjika mwezi Machi mwaka huu.
Rais Joseph Kabila
Orodha ya watu 60 waliotangazwa katika nafasi za mawaziri na manaibu waziri inajumuisha majina mengi yaliyokuwa katika mabaraza yaliyotangulia, na wizara muhimu kama ya mambo ya nje, mambo ya ndani, sheria na migodi zimekwenda kwa wapambe wa Rais Kabila.
Baraza jipya litakabiliwa na changamoto kubwa, zikiwemo kuporomoka kwa thamani ya sarafu ya Faranga, na uhaba wa raslimali inayohitajika kuandaa uchaguzi mkuu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.
CHANZO: DW
No comments:
Post a Comment