Meneja Uuhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando (kulia) na Ofisa huduma kwa wateja wa Airtel, Veronica Valentine (kushoto) wakionesha simu aina ya ZTE na Motorola katika banda la Airtel lililoko katika viwanja vya maonesho ya biashara maarufu kama sabasaba, simu hizo zitauzwa kwa bei ya ofa ya shilingi 16,000 tu na mteja ataunganishwa na kufurushi cha muda wa maongezi kwa mwezi mzima cha shilingi 10,000 BURE. Katikati ni Ofisa huduma kwa wateja wa Airtel, Tumwidike Michael
Kampuni
ya simu za mkononi ya Airtel imetangaza ofa kabambe wakati wote wa
maonyesho ya biashara ya sabasaba mwaka huu zitakazowawezesha wateja
wake na wale wapya kuunganishwa na huduma za mtandao kwa gharama nafuu
na pia kujipatia simu bomba kwa bei nafuu.
Akiongea
na waandishi wa habari katika banda la Airtel lililopo viwanja vya
sabasaba Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando alisema “dhamira
yetu Airtel ni kuendelea kuunganisha jamii kwa bidhaa na huduma, hivyo
kwa msimu huu maonesho ya saba saba tutatoa ofa nyingi sana ikiwemo
simu aina ya ZTE GS 500, Motorola C113, Motorola F3 na Motorola C117 kwa
sh. 16,000 tu na mteja akishanunua ataunganishwa
na bando la sh. 10,000 litakalodumu kwa muda wa mwezi mmoja”
“Unaweza
ukaona hapo gharama ya simu inakuwa nafuu na kisha unaunganishwa na
kifurushi cha mwezi mzima BURE kuongea na ndugu, jamaa, na marafiki
huku ukifaidi huduma zingine za Airtel” alieleza Mmbando
Katika
banda letu ndani ya saba saba mwaka huu pia huduma zitakazopatikana ni
pamoja na kubadilisha laini, huduma za Airtel Money, simu za
smartphone
za kisasa na origino, huduma ya Timiza Vicoba, kuelekezwa jinsi
yakusoma masomo ya ufundi kwa njia ya simu VETA kupitia Vsomo pamoja na
kujua jinsi yakufungua biashara ya Duka la Airtel popote na jinsi ya
kupata faida yako”
Mmbando
alisema kuwa “Airtel imekuwa ni desturi yetu kuleta huduma na bidhaa
zetu katika maonyesho haya ya biashara kila mwaka na kukutana na wateja
wetu ana kwa ana ili kutoa elimu zaidi kuhusu huduma zetu mpya na za
kibunifu tunazozitoa kila mwaka”.
“Natoa
wito kwa Watanzania kutembelea banda letu na kujipatia simu huduma za
kimtandao zote kwa gharama nafuu na vilevile kukutana na watoa huduma
wetu na kupata elimu juu ya huduma mbalimbali ikiwemo Kupata maelekezo
ya kupata mikopo ya vikundi kupitia huduma ya Timiza vikoba. Kupata
maelekezo ya kuweza kufanya biashara za Airtel kokote Tanzania kupitia
mfumo wa Maduka ya Airtel AMSHA pamoja na
huduma nyingine nyingi” aliongeza Mmbando.
SHARE
No comments:
Post a Comment