TRA

TRA

Friday, June 16, 2017

Alhaj Mzee Yusuph afunguka kilichosababisha kuacha muziki

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Aliyekuwa mwimbaji wa muziki wa Taarabu Mzee Yusuph ambaye kwa sasa anafahamika kama Alhaj Mzee Yusuph amefunguka kuhusu kuacha kwake muziki na kufanya toba ili kurudi kuwa muumini na kutoa daa’wa.

Akizungumza kwenye  Clouds FM Juni 15, 2017 Alhaj Mzee Yusuph amegusia pia jinsi maneno ya watu yalivyofuata baada ya kutangaza na hatimaye kuacha kabisa muziki huku akielezea namna alivyokuwa anakataza watu kwenye Kundi lake wasitende maovu.

"Mimi nimeacha muziki kwa sababu nataka kuwa Muumuni wa Dini ya Kiislamu na kumfuata Mtume Muhammad (SAW). Nilipopata nafasi ya kwenda kuhiji Makka na kushika Al Kaaba nilimuomba Mwenyezi Mungu anisamehe makosa yangu.

“Nilipoanza kubadilika nilikuwa nakataza pombe kwenye Band yangu. Siku nisiyowepo walikuwa wanasema Simba leo hayupo. Nilipokuwa nakataza haya mambo wengi walikuwa wakiniambia kwa nini nisifungue Madrasa. Kubadilika kwangu niliachana kwanza na starehe magoma kwanza maana ilikuwa ni kama kunywa maji tu unaposikia kiu.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger