TRA

TRA

Wednesday, June 14, 2017

Aspirin ni hatari kwa binadamu

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 
Watu walio na umri wa zaidi ya miaka 75 ambao hutumia dawa aina ya Aspirin baada ya kupata kiharusi au maradhi ya moyo wako hatarini kupata matatizo ya kuvuja damu tumboni, Shirika la utafiti wa kitabibu Lancet limeeleza.

 Vidonge vya Aspirin ni hatari kwa watumiaji wa umri wa zaidi ya miaka 75

Wanasayansi wanasema, kupunguza athari hizo , watu walio na umri mkubwa wanapaswa kumeza dawa za kuzuia maradhi ya tumboni (PPI)

Lakini wamesisitiza kuwa Aspirin ina faida muhimu kama vile kuzuia maradhi ya moyo.

Utafiti wa kitabibu nchini Uingereza umeashiria kwamba kumeza vidonge vya dawa aina ya Aspirin kuna athari kubwa zaidi kuliko ilivyodhaniwa hapo awali hususan kwa watu wenye umri mkubwa.

 Dawa hiyo ambayo inatumiwa kuzuia mshtuko wa moyo na maradhi ya kiharusi imehusishwa kwa siku nyingi kusababisha matatizo ya uvujaji wa damu ndani ya tumbo.

Wataalam hao wametahadharisha kuwa kusitisha ghafla matumizi ya Aspirin kunaweza kuleta madhara, hivyo mtu yeyote anashauriwa kupata ushauri wa Daktari ikiwa anatakiwa kubadili dawa.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger