TRA

TRA

Thursday, June 22, 2017

JEZI NAMBA 7 YAZUA TAHARUKI ARSENAL, SANCHEZ AWA GUMZO

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !




Mashabiki wa Arsenal wameonekana kushitushwa na jezi namba 7 za msimu ujao ambayo inawaonyesha kuwa mshambuliaji wao Alexis Sanchez, ameishaagana nao.

Arsenal imetangaza jezi mpya, lakini kinachoonyesha kuwashangaza ni kwamba katika jezi hizo, yenye namba 7 imeandikwa jina la Welbeck badala ya Sanchez.

Wakati masabiki walipoanza kununua jezi hizo kwa pauni 77, takribani Sh 280,000 wamekuwa wakishangazwa na hilo.



Hata hivyo, Arsenal bado haijatangaza rasmi kama Sanchez anaondoka au amebadilishiwa jezi tu. Tayari raia huyo wa Chile alishaonyesha kwamba amenuia kuondoka na Bayern Munich na Chelsea zilikuwa kati ya timu zinazomuania kwa udi na uvumba.



Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger