NA K-VIS BLOG/Mashirika ya Habari
WATU kadhaa
wameuawa na zaidi wengi 50 kujeruhiwa kutokana na moto mkubwa ambao umezuka kwenye
jengo la ghrorofa 24 Grenfell Tower la makazi ya watu jijini London, Uingereza
leo Jumatano Juni 14, 2017.
Meya
wa jiji hilo Mstahiki Sadiq Khan amesema idadi kubwa ya watu
wamejeruhiwa na watu wengine ambao idadi yao haijajulikana wameuawa.
Kikosi
cha zimamoto na uokoaji jijini London, kimetuma kwa uchache wahandisi wa moto
40, magari ya kubeba wagonjwa, (Ambulance), zipatazo 20 na zaidi ya askari wa
zimamoto na uokoaji wapatao 200.
Mwakilishi
wa kikosi cha zimaoto na uokoaji jijini London amesema kuna idadi kubwa ya
waliokumbwa na kadhia hiyo ya moto lakini amekataa kusema ni watu wangapi
wameuawa.
SHARE
No comments:
Post a Comment