Mmoja wa Wananchi akiweka saini ya
kielektroniki katika zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa
linaloendela katika Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa – NIDA
ndani ya Viwanja Maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (SABASABA)
Mmoja wa Wananchi akiweka saini ya
kielektroniki katika zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa
linaloendela katika Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa – NIDA
ndani ya Viwanja Maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (SABASABA)
Ofisa usajili Mamalaka ya
Vitambulisho vya Taifa – NIDA Ndg. Daniel Katondo akitoa maelekezo ya
namna ya kujaza fomu kwa mmoja wa Wananchi waliojitokeza katika zoezi la
usajili ndani ya Banda la NIDA katika Maonyesho ya 41 ya kibiashara
maarufu kama sabasaba.
Wananchi wakipatiwa huduma
mbalimbali Ndani ya Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa – NIDA
ikiwemo Elimu kuhusu umuhimu wa kitambulisho cha Taifa. Pichani Afisa
Uhamiaji Bw. Jamal Kaoneka akimhakiki mmoja wa Wananchi wakati wa
kukamilisha Tararibu za Usajili.
Huduma za Usajili zikiendelea
kutolewa kwenye Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi
waishio Mkoa wa Dar-es-Salaam, pamoja na kupatiwa taarifa za hatua za
Maombi ya Vitambulisho yalipofikia kwa wale waliokwisha kujisajili.
Mmoja wa Wananchi waliojitokeza
katika Banda la Mamlaka ya Vitambulihso akipatiwa maelezo mbalimbali
hukusu Usajili wa Vitambulisho vya Taifa pamoja na Elimu juu ya umuhimu
wa Vitambulisho vya Taifa pamoja na Matumizi yake.
………………………
Wananchi kutoka viunga mbalimbali
vya Mkoa wa Dar-es-salaam wameendelea kumiminika katika Banda la
Maonyesho la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) lililopo kwenye
hema la Jakaya Mrisho Kikwete kuchangamkia Ofa ya Kusajiliwa na kupata
Vitambulisho vya Taifa, ndani ya siku za Maonyesho hayo yanayoendelea
katika Viwanja ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Mbali na kusajiliwa; baadhi
wamejitokeza kupata taarifa za Usajili waliofanya siku za nyuma na
kujifunza zaidi kuhusu matumizi na faida za Vitambulisho vya Taifa
ambavyo vimeanza kutumika katika huduma mbalimbali nchini zinazotolewa
na baadhi ya Taasisi na Mashirika ya Serikali yakiwemo makampuni ya
Simu.
Akizungumza kupitia vyombo
mbalimbali vya Habari leo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano (NIDA),
Bi. Rose J. Mdami amewataka wananchi kutumia vizuri fursa hii hususani
wananchi na wakazi wa mkoa wa Dar-es-salaam ambao hawajasajiliwa
Vitambulisho vya Taifa; kwani kwa kipindi hiki cha Sabasaba wametoa
kipaumbele kwa wananchi hao ili kupanua wigo wa matumizi mapana ya
Vitambulisho hivyo kielektroniki.
“Nasisitiza wananchi wa
Dar-es-salaam ambao hawajasajiliwa; wajitokeze wakiwa na viambatisho
muhimu vya kuwatambulisha mathalani Cheti cha Kuzaliwa, Vyeti vya Shule,
Pasi ya Kusafiria(Passport), Kadi ya Kupigia Kura, TIN namba, Kadi ya
Bima ya Afya, Kitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi, Leseni ya Udereva na
Kadi ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii. Kuwa na Viambatisho vingi zaidi ni
kutambulika kwa haraka zaidi” Alisitiza
Kwa mujibu wa Bi. Rose
Kitambulisho hicho ni bure; na huduma hii ya kupata Kitambulisho ndani
ya siku za maonyesho ni kwa siku saba tu za mwanzo yaani hadi tarehe
07/07/2017, baada ya hapo utaratibu wa kawaida wa kuwasajili wananchi
utaendelea. Wananchi pia wameshauriwa kuanza taratibu za kujaza fomu za
maombo ya Usajili kwenye Serikali za Mitaa wanakoishi na kugonga mhuri
kabla ya kufika kwenye Banda la NIDA ili kurahisisha zoezi.
NIDA inashiriki kwa mara ya
pili maonyesho ya Kimataifa ya Sabasaba ikiwa imekusudia kuwaelimisha
wananchi namna gani Mfumo wa Utambuzi na Usajili wa Watu ni ngazi katika
kufikia malengo mapana ya Serikali ya Ukuzaji Biashara na Maendeleo ya
Viwanda kama Kauli mbiu ya Maonyesho hayo inavyosema “Ukuzaji wa Biashara kwa Maendeleo ya Viwanda” .
Afisa usajili Mamalaka ya
Vitambulisho vya Taifa – NIDA Ndg. Daniel Katondo akitoa maelekezo ya
namna ya kujaza fomu kwa mmoja wa Wananchi waliojitokeza katika zoezi la
usajili ndani ya Banda la NIDA katika Maonyesho ya 41 ya kibiashara
maarufu kama sabasaba.
Wananchi wakipatiwa huduma
mbalimbali Ndani ya Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa – NIDA
ikiwemo Elimu kuhusu umuhimu wa kitambulisho cha Taifa. Pichani Afisa
Uhamiaji Bw. Jamal Kaoneka akimhakiki mmoja wa Wananchi wakati wa
kukamilisha Tararibu za Usajili.
Huduma za Usajili zikiendelea
kutolewa kwenye Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi
waishio Mkoa wa Dar-es-Salaam, pamoja na kupatiwa taarifa za hatua za
Maombi ya Vitambulisho yalipofikia kwa wale waliokwisha kujisajili.
Mmoja wa Wananchi waliojitokeza
katika Banda la Mamlaka ya Vitambulihso akipatiwa maelezo mbalimbali
hukusu Usajili wa Vitambulisho vya Taifa pamoja na Elimu juu ya umuhimu
wa Vitambulisho vya Taifa pamoja na Matumizi yake.
………………………
Wananchi kutoka viunga mbalimbali
vya Mkoa wa Dar-es-salaam wameendelea kumiminika katika Banda la
Maonyesho la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) lililopo kwenye
hema la Jakaya Mrisho Kikwete kuchangamkia Ofa ya Kusajiliwa na kupata
Vitambulisho vya Taifa, ndani ya siku za Maonyesho hayo yanayoendelea
katika Viwanja ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Mbali na kusajiliwa; baadhi
wamejitokeza kupata taarifa za Usajili waliofanya siku za nyuma na
kujifunza zaidi kuhusu matumizi na faida za Vitambulisho vya Taifa
ambavyo vimeanza kutumika katika huduma mbalimbali nchini zinazotolewa
na baadhi ya Taasisi na Mashirika ya Serikali yakiwemo makampuni ya
Simu.
Akizungumza kupitia vyombo
mbalimbali vya Habari leo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano (NIDA),
Bi. Rose J. Mdami amewataka wananchi kutumia vizuri fursa hii hususani
wananchi na wakazi wa mkoa wa Dar-es-salaam ambao hawajasajiliwa
Vitambulisho vya Taifa; kwani kwa kipindi hiki cha Sabasaba wametoa
kipaumbele kwa wananchi hao ili kupanua wigo wa matumizi mapana ya
Vitambulisho hivyo kielektroniki.
“Nasisitiza wananchi wa
Dar-es-salaam ambao hawajasajiliwa; wajitokeze wakiwa na viambatisho
muhimu vya kuwatambulisha mathalani Cheti cha Kuzaliwa, Vyeti vya Shule,
Pasi ya Kusafiria(Passport), Kadi ya Kupigia Kura, TIN namba, Kadi ya
Bima ya Afya, Kitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi, Leseni ya Udereva na
Kadi ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii. Kuwa na Viambatisho vingi zaidi ni
kutambulika kwa haraka zaidi” Alisitiza
Kwa mujibu wa Bi. Rose
Kitambulisho hicho ni bure; na huduma hii ya kupata Kitambulisho ndani
ya siku za maonyesho ni kwa siku saba tu za mwanzo yaani hadi tarehe
07/07/2017, baada ya hapo utaratibu wa kawaida wa kuwasajili wananchi
utaendelea. Wananchi pia wameshauriwa kuanza taratibu za kujaza fomu za
maombo ya Usajili kwenye Serikali za Mitaa wanakoishi na kugonga mhuri
kabla ya kufika kwenye Banda la NIDA ili kurahisisha zoezi.
NIDA inashiriki kwa mara ya
pili maonyesho ya Kimataifa ya Sabasaba ikiwa imekusudia kuwaelimisha
wananchi namna gani Mfumo wa Utambuzi na Usajili wa Watu ni ngazi katika
kufikia malengo mapana ya Serikali ya Ukuzaji Biashara na Maendeleo ya
Viwanda kama Kauli mbiu ya Maonyesho hayo inavyosema “Ukuzaji wa Biashara kwa Maendeleo ya Viwanda” .
SHARE
No comments:
Post a Comment