TRA

TRA

Thursday, June 29, 2017

Kumekucha Sabasaba. Unawafahamu PROPERTY INTERNATIONAL nenda uone huduma zao

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


P1
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Property International Bw. A. Haleem akishauriana jambo na Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Bw. Masoud Alawi katika banda la kampuni hiyo lililoko katika viwanja vya TANTRADE Barabara ya Kirwa jijini Dar es salaam ambapo maonyesho ya biashara ya Sabasaba yanaendelea kuanzia jana na yataendelea kwa muda wa siku kumi .
Kampuni hiyo inajishughulisha na upimaji wa viwanja na kuuza kupitia mabenki mbalimbali ambayo wameingia mkatataba nayo katika mpango huo  mabenki  yataweza kumlipia mteja wa kiwanja kwa mkopo alafu mteja atarejesha rejesho kidogokidogo mpaka atakapomaliza mkopo wake na kukabidhiwa hati ya kumiliki kiwanja chake muhimu mteja atatakiwa kulipa asilimia 5 mpaka 20 mwanzo wa mkopo wake kulingana na makubaliano ya kiwanja anachohitaji.
Kampuni hiyo pia inajishughulisha na ujenzi wa nyumba na uuzaji wa vifaa mbalimbali vya ujenzi ikiwa ni pamoja na uchimbaji wa visima vya maji, Katikati katika picha ni Bw. Suleiman Abdallah Mchoraji wa ramani za majengo  kutoka kampuni ya Property International.
P2
Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Bw. Masoud Alawi akitoa maelezo kwa wateja waliotembelea katika banda hilo leo ili kujionea mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na bidhaa zinazopatikana katika banda hilo kulia ni Bw. Suleiman Abdallah Mchoraji wa ramani za majengo  kutoka kampuni ya Property International.
P03
Bw. Suleiman Abdallah Mchoraji wa ramani za majengo  kutoka kampuni ya Property International akitoa maelezo kwa Bw. Mahuna Tendwa kutoka Suma JKT aliyetembelea katika banda la Property International katikati ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Bw. Masoud Alawi.
P3
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Property International Bw. A. Haleem akishirikiana na mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo kutoa maelezo na kuonyesha ramani za viwanja vilivyopo jijini Dar es salaam na mkoa wa Pwani kwa wateja mbalimbali waliotembelea banda hilo.
P4
Mmoja wa wafanyakazi akiwa katika banda hilo ili kutoa huduma kwa wateja wanaotembelea katika maonyesho hayo.
P5
Wateja wakiendelea kupata huduma katika banda hilo.
P6
Baadhi ya wafanyakazi wakiwa na nyuso za bashasha wakati wakikaribisha wateja katika banda ka kampuni hiyo.
P7
Baadhi ya bidhaa zinazoonyeshwa katika banda hilo.
P8
Bw. Abdul Msalam Mtaalam wa masuala ya uchimbaji wa visima kutoka kampuni hiyo akiwa katika eneo lake kama zinavyoo pampu mbalimbali maalum kwa ajili ya visima virefu na vifupi.
P9
Muonekano wa Banda la Property International linavyoonekana.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger