Moshi. Wananchi wa mtaa wa Fonga kata ya Pasua,
mkoani Kilimanjaro wamemwomba Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendelo ya
Makazi, William Lukuvi kuingilia kati bomoabomoa inayoendelea mkoani
humo.
Wananchi hao walisema kuwa maeneo yaliyowekwa alama ya X yana hati miliki ambayo walipewa na Wizara ya Ardhi.
Hata hivyo mmoja wa waathirika hao, Charles Msuya amesema wao sio wavamizi na wamepewa kihalali maeneo hayo na Manispaa ya Moshi
Amesema wamekua wakilipia majengo hayo kila mwaka tangia
wamilikishwe maeneo hayo rasmi na Manispaa.
“Nikirejea
nyuma, Oktoba, 2007 kipindi cha Waziri wa Ardhi wakati huo Rais John
Magufuli alikuja katika maeneo yetu na kuhutubia wananchi na moja wapo
ya vitu alivyoagiza ni mkurugenzi chini ya mkuu wa mkoa aliyekuepo
kipindi hicho kuhakikisha wananchi wa eneo hilo wanapewa hati miliki na
ndiyo watu walianza kujenga na hadi sasa wanaendelea kujenga.
Antony
Kisinga ambaye ni mmiliki wa majengo mbalimbali ya biashara eneo hilo
amesema kitendo kinachofanywa na Kampuni ya Reli ni uonevu kutokana na
kwamba miaka 10 iliyopota hajawahi kufuatwa na mtu yeyote kuhusiana na
eneo hilo.
“Sasa napewa notisi ya kuvunja nyumba kwa
siku 30 kwa mtu ambaye hajawahi kuninyooshea kidole wala hajawahi
kuongea na mimi nilishtuka sana, hiki ni kitendo cha kibabe,”amesema
Kisinga.
Hata hivyo, alisema kuwa kutokana na kwamba ana nyaraka zote za umiliki wa eneo hilo na yeye sio mvamizi.
Kwa
upande wake diwani wa kata hiyo, Charles Mkalakala amesema bomoabomoa
hiyo imewaathiri watu wengi kutokana na eneo hilo kubadilishwa matumizi
na Manispaa ya Moshi.
“Ni vizuri Serikali ikaangalia kuhusiana na zoezi hili kutokana na
kwamba
kila mu ana hati miliki na kwamba hati ni mali ya Serikali, cha msingi
Serikali iangalie kama walikubali kubadilisha matumizi basi wawaachie
wananchi maeneo haya,”amesema Mkalakala.
Zoezi la
bomoabomoa lilianza kutikisa Moshi baada ya Kampuni Hodhi ya Rasilimali
za Reli(Rahco), kutia timu mkoani hapa na kuvunja zaidi ya nyumba 500
SHARE
No comments:
Post a Comment