Katibu mkuu wa shirika la kujihami
la nchi za magharibi (Nato), Jens Stoltenberg, amesema kuwa mpango wa
nyuklia wa korea Kaskazini na tisho kwa dunia nzima.
Kipengee cha tano cha makubaliano ya Nato kinasema kuwa shambulizi dhidi ya mwanachama mmoja ni shambulizi dhidi ya wanachama wote.
Guam ambacho ni kisiwa himaya ya Marekani kilicho bahari ya Pacific ni kituo muhimu cha kijeshi na kimetishiwa mara kwa mara na Korea Kaskazini.
- Korea Kaskazini yasifia jaribio jingine la nyuklia
- Korea Kusini yafanya majaribio ya makombora kujibu majaribio ya Korea Kaskazini
- Meli za kivita za Urusi 'kukwepa' Uhispania
- Korea Kaskazini yashutumiwa kwa kulipua bomu
Alitoa wito wa Korea Kaskazini kuacha kuunda zana za nyuklia akisema kuwa huo ni ukiukaji mkubwa wa maazimio ya Umoja wa Mataifa,na tisho kwa amani ya dunia.
Matamshi ya Bw Stoletnberg yanakuja wakati wanachama wa baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa wanatofautiana kuhusu njia za kuukabili mzozo wa Korea Kaskazini kufuatia hatua yake ya hivi punde ya kufanyia jaribio kombora kupitia anga ya Japan.
CHANZO: BBC
SHARE
No comments:
Post a Comment