Tigo inatoa dakika 100 za muda wa maongezi, SMS 100 SMS na and 100 Mbs za data kwa manunuzi yote ya tiketi kupitia TigoPesa
Jumatatu 4 Septemba, 2017- Huku ikiwa imebakia siku chache tu kabla ya onesho la kwanza la msimu wa Tigo Fiesta 2017 – Tumekusomaa kufanyika jijini Arusha, wadhamini wakuu kampuni ya Tigo inazidi kutoa ofa kabambe kwa wateja wote wa Tigo watakaonunua tiketi zao za awali kupitia huduma ya TigoPesa.
Tigo inatoa dakika 100 za bure, SMS 100 za bure, na kifurushi cha 100Mbs cha data bure kwa wateja wote wa Tigo watakaonunua tiketi zaoTigo Fiesta 2017 - Tumekusomaa kupitia huduma ya TigoPesa.
Akitangaza ofa hiyo murwa jijini Dar es Salaam jana, Mkuu Mtendaji wa Huduma za Masoko wa Tigo, William Mpinga alisema kuwa ofa hii mpya ya dakika 100 za muda wa maongezi, SMS 100 na 100Mbs za data inaenda sambamba na ofa iliyopo sasa ya punguzo ya bei asilimia 10% kwa tiketi zote za awali za Tigo Fiesta 2017 zitakazonunuliwa kupitia Tigo Pesa au huduma ya kuhamisha fedha ya mitandao mingine yote ya simu nchini.
SHARE
No comments:
Post a Comment