NA WAMJW-DAR ES SALAAM.
WIZARA
ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto imepokea shilingi
Bilioni 227.76 kutoka kwenye mfuko wa pamoja (Health Basket Fund) kwa
ajili ya kufadhili shughuli mbalimbali za sekta ya afya nchini.
Akizungumza
na Waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam wakati wa kupokea fedha
hizo , Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa
fedha hizo zitaelekezwa katika uboreshaji wa huduma za afya nchini.“Fedha
hizi zitasaidia pia kutoa huduma za chanjo kwani ni afua muhimu kwa
wananchi hususan katika kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto
wenye umri chini ya miaka mitano nchini” alisema Dkt. Ulisubisya.
Aidha
Dkt. Ulisubisya amesema kuwa kwa mara ya kwanza wameamua kupeleka fedha
hizo moja kwa moja kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili kuepuka
changamoto za vituo hivyo kukosa dawa muhimu mara kwa mara.Mbali
na hayo Dkt. Ulisubisya alisema kuwa asilimia 90 ya fedha hizo zinaenda
moja kwa moja kwenye vituo vinavyotolea huduma za afya vya ngazi ya
Halmashauri na asilimia 10 inatumika kwa ajili ya shughuli mbalimbali za
usimamizi wa kisera katika sekta ya afya nchini.
Aidha
Dkt. Ulisubisya amesema kuwa fedha hizo pia zitasaidia katika
kuimarisha miundombinu katika vituo vya afya na zahanati ili viweze
kutoa huduma za upasuaji wa dharura kwa ajili ya akina mama wajawazito
wanaokabiliwa na uzazi pingamizi.
Kwa
upande wake Balozi wa Denmark nchini Tanzania Bw. Einar Jensen kwea
niaba ya wadau wa mfuko huo amesema kuwa mbali na Fedha hizo
kushughulikia maswala ya afya nchini hapa pia zitakuwa na shughuli
mbalimbali za maendeleo .
“Mbali
na kushughulikia masuala ya afya pia napendekeza fedha hizi zihusike
katika kuhudumia wakimbizi wanaongia Tanzania hasa katika maeneo ya
Kigoma na Kibondo” alisema Bw. Jensen.
Picha
ya Pamoja ya makabidhiano ya mkataba wa mfuko wa pamoja (Health Basket
Fund) kwa ajili ya kufadhili shughuli mbalimbali za sekta ya afya nchini
ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Mh. Dotto James
na Balozi wa Denmark nchini Tanzania Bw. Einar katika kikao
kilichofanyika ofisi ndogo za Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es
salaam,wakwanza kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki
Ulisubisya
Balozi wa Denmark nchini Tanzania Bw. Einar Jensen akisisitiza jambo katika kikao cha makabidhiano ya mkataba wa mfuko wa pamoja (Health Basket Fund), kilichofanyika mapema leo katika ofisi ndogo za Wizaraya Fedha na Mipango jijini Dar es salaam.
Watumishi wa Serikali wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya wakifuatilia kwa karibu majadiliano katika kikao cha makabidhiano ya mkataba wa mfuko wa pamoja (Health Basket Fund) kwa ajili ya kufadhili shughuli mbalimbali za sekta ya afya nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akisaini mkataba wa mfuko wa pamoja (Health Basket Fund) kwa ajili ya kufadhili shughuli mbalimbali za sekta ya afya nchini, tukio lililofanyika katika ofisi ndogo za Wizara ya Fedha na Mipango leo jijini Dar es salaam.
SHARE
No comments:
Post a Comment