TRA

TRA

Wednesday, October 4, 2017

STARTIMES KUONYESHA KOMBE LA DUNIA MUBASHARA KUTOKA URUSI 2018

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Mkurugenzi na Uendeshaji wa StarTimes Tanzania, Carter Luoh (katikati) akizungumzia juu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja. Kulia kwake ni Meneja wa Uendeshaji wa StarTimes Tanzania, Gasper Ngowi na Meneja Huduma kwa Wateja StarTimes, Henry Ngailo.
Kampuni ya StarTimes Tanzania inayouza King’amuzi cha StraTimes, imetangaza kuwa, imepata haki ya kuonyesha michuano ya Kombe la Dunia ambayo itafanyika mwakani nchini Urusi.
Hayo yamesemwa na Meneja wa Uendeshaji wa StarTimes Tanzania, Gasper Ngowi, katika hafla ya kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja ambayo huadhimishwa kila wiki ya kwanza ya mwezi Oktoba.
“Tunapenda kuwataarifu wateja wetu kuwa king’amuzi chetu cha StarTimes kimepata haki za kuonyesha michuano ya Kombe la Dunia ambayo itafanyika mwakani nchini Urusi, hivyo ni wakati wao sasa kuchangamkia fursa hiyo kwa kulipia ving’amuzi vyao,” alisema Ngowi.
Naye Mkurugenzi na Uendeshaji wa StarTimes Tanzania, Carter Luo, amesema: “Katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja, tumekuja na kitu kipya ambapo tumeongeza chaneli kwenye king’amuzi chetu kwa ajili ya kuwapa burudani zaidi wateja wetu kwani tunawajali sana.”
Pia Luo amesema ili kuwafikia wateja wao kwa haraka na kuwatatulia matatizo yao, katika kitengo chao cha huduma kwa wateja wameongeza watu na kufikia 300 ambapo wateja wao watakuwa wakiwasiliana nao kwa namba 0764700800 na 0677700800.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger