TRA

TRA

Saturday, February 17, 2018

DK. KIGWANGALLA AMALIZA MGOGORO WA HIFADHI NA WANANCHI WILAYANI RUFIJI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Na Hamza Temba - Rufiji, Pwani

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amemaliza mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya miaka minne baina ya Hifadhi ya Msitu wa Utete na vitongoji vinavyopakana na hifadhi hiyo vya Siasa, Nyawanje, Kindwitwi na Utunge katika wilaya ya Rufiji mkoani Pwani.
Dk. Kigwangalla amemaliza mgogoro huo kwa kumuagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Prof. Dos Santos Silayo kuunda timu ya wataalamu watakaoshirikiana na wataalamu wa mkoa wa Pwani na wilaya ya Rufiji kwa ajili ya kufanya tathmini ya eneo lenye mgogoro na kuanzisha mchakato wa kisheria wa kurekebisha mipaka ya eneo hilo na hatimaye kuligawa kwa wananchi.
Dk. Kigwangalla ametoa agizo hilo jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Utete, wilaya ya Rufiji mkoani Pwani wakati wa ziara yake ya kikazi ya kutatua migogoro baina ya hifadhi na wananchi mkoani humo
                             Dk Hamis Kigwangalla
“Naagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, uunde timu ya wataalam waje washirikiane na wataalam wa mkoa na wilaya, wafanye tathmini kwenye lile eneo ambalo wananchi wamekuwa wakilima kabla hata msitu haujawa ‘gazerted’ (haujatagazwa) kuwa hifadhi ili muone ni kwa kiasi gani mnaweza mkamega eneo na kulirudisha kwa wananchi ili waweze kuendelea na kilimo,” aliagiza Dk. Kigwangalla.
Ameagiza pia kamati hiyo ifanye tathmini ya eneo la chemchem ambalo ni sehemu ya hifadhi hiyo ambalo limevamiwa kwa kiasi kikubwa na makazi ya wananchi ili waweze kurekebisha mipaka yake na hatimaye wananchi wabaki na eneo lao la makazi na eneo litakalobakia liendelee kuhifadhiwa.
“Kamati hiyo pia ije ifanye tahtmini inawezaje kuhamisha mipaka ya hifadhi ili kupisha zile nyumba ambazo zimeshajengwa pale kwa sasa na hapo sasa wananchi wawe hawana mgogoro na hifadhi, waishi kwenye eneo lao na waiache hifadhi upande wa pili, lakini sasa waishi kwa mujibu wa sheria kuliko ilivyo hivi sasa tunavyowachukulia kama wavamizi;” alisema Dk. Kigwangalla.
Aidha Dk. Kigwangalla ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji kutafuta eneo mbadala la msitu ambalo ni mali ya vijiji likabidhiwe kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ili liweze kuhifadhiwa ikiwa ni fidia ya eneo hilo la Hifadhi ya Msitu wa Utete litakalokabidhiwa kwa wananchi kwa ajili ya kilimo na makazi.
Mbali na maagizo hayo Dk. Kigwangalla ameagiza pia wananchi waliolima kwenye bonde katika Hifadhi hiyo wasiondolewe katika msimu huu wa kilimo wakati zoezi la uwekaji wa mipaka likiwa linaendelea.
Hifadhi ya Msitu wa Utete ilianzishwa kwa tangazo la Serikali Na. 1cap 132p 1351 la tarehe 1 Oktoba, 1957 ikiwa na jumla ya ekari 2,346. Desemba 2015 msitu huo ulipimwa tena na kuchorewa ramani.
Wananchi wanaozunguka hifadhi hiyo wamedai kuwepo katika baadhi ya maeneo hayo ya hifadhi hata kabla ya kuanzishwa kwa hifadhi hiyo, hivyo wameiomba Serikali iwamegee maeneo katika hifadhi hiyo ili waweze kuendeleza shughuli zao za kilimo na makazi.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger