TRA

TRA

Tuesday, February 27, 2018

IGP Sirro Atoa ONYO Kali Waliopanga Kuandamana Nchi Nzima

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !





Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro ametoa onyo akisema wamejiweka tayari kukabiliana na watu, wakiwemo wanasiasa wanaohamasishana kuandamana nchi nzima kinyume cha sheria.


Sirro alisema hayo jana mjini Bariadi baada ya kukutana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Simiyu alikokuwa ziarani kukagua utayari wa askari wa jeshi hilo.


“Kuna makundi ya vijana wanaojiita wana mapinduzi wanahamasishana na kupanga kuandamana nchi nzima wakiratibiwa na chama kimoja cha siasa, tumejipanga kuwadhibiti na tutawakamata wote bila kujali vyeo na madaraka yao,” alisema.


Sirro aliwataka wazazi na walezi kuwaonya na kuwazuia vijana wao kushiriki maandamano yasiyo na kibali kwa sababu hakuna atakayevunja sheria atakayesalimika bila kuchukuliwa hatua stahiki.


“Kuvunja sheria ni jambo rahisi lakini madhara yake ni makubwa. Wananchi wasijiingize kwenye mambo yakiwemo uhalifu ambayo mwishowe huwagharimu,” alisema.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger