Vero Ignatus - Moshi Kilimanjaro.
Chama cha 
Karate Mkoa wa Kilimanjaro wanaiomba serikali kutupia macho kwenye 
mchezo huo kwani imekuwa ikiwasahau ukizingatia mchezo huo ni michezo 
kama ulivyo mingine  na kwamba mchezo huo umekuwa ukifundishwa pia 
katika majeshi mbalimbali hapa nchini.
Hayo yamesemwa nakapteni wa timu na   katibu msaidizi wa chama cha 
Katrate mkoa wa Kilimanjaro bwana  Wembo  Hamisi katika viwanja vya 
mazowezi mkoani hapo  na amekusema kuwa wamekuwa wakikwama mara 
wanapohitajika kwenye mechi za kirafiki,ndani na nje ya nchi kwasababu 
hawana sapoti kutoka serikalini na wafadhili. 
 Aidha
 amesema kuwa Karate ni mchezo ambao mtu yeyote anaweza kuucheza na 
akatengeneza  afya ya mwili,na mchezo huo ni wa kawaida kama ilivyo 
michezo mingine kama mpira wa miguu amewataka watu wote kujitokeza kwa 
wingi kujiunga katika mchezo huo wa Karate kwa sifa kuu ya karate ni 
nidhamu.
Sambamba na hayo bwana Wembo amesema kuwa katika mchezo huo wapo 
wanawake na ameiomba jamii waondokane na ile dhana potofu kwamba 
mwanamke akicheza mchezo huo wa Karate hawezi kupata mtoto na kufanya 
shughuli nyingine za kijamii amesema huo ni upotoshaji kwani mwanamke 
anao uwezo wa kupata mtoto kama walivyo wengine na anatengeneza afaya 
nzuri kabisa. 
Aidha
 amesesema kuwa mchezo huo wa Karate kwa historia umeanzishwa miaka 
mingi  kwa mkoa wa Kilimanjaro chama cha karate kina takribani miaka 
saba  sasa tangia  kuanzishwa kwa chama hicho,na baadae wakaunda 
shirikisho la Karate nchini Tanzania ambapo inajumuisha michezo yote ya 
karate ,ambapo januari 30 watakuwa na tamasha la Karate la 
kuwatambulisha wachezaji wa timu litakalofanyika mkoani hapo katika 
ukumbi wa shule ya msingi Mwenge. 
Katibu
 huyo  ameinisha ratiba yao ndani ya  miezi  sita ambapo watafanya 
matamasha mbalimbali ikwemo februari 13/2016 watafanya  tamasha wilayani
  Same katika ukumbi wa kimweli  same  mjini, machi 24-26,  mashindano  
ya  mchezo wa GOJUKAI KARATE  ya  Afrika Mashariki,  Kampala Uganda , 
aprili  30  mashindano  ya  GOJUKAI  Karate  ya  wazi ya kuuenzi mlima 
Kilimanjaro ambapo  watashiriki watoto  wenye  umri  wa  kati  na watu  
wazima  yatafanyika  Moshi.
Mwisho
  ni  Tamasha  la  shukrani litakalofanyika  mei 16 hapo hapo  Moshi  
Kilimanjaro.
Kwa mkoa wa Kilimanjaro mchezo wa karate unaochezwa unajulikana kama 
Gojukai Stayle, ambayo ilianzishwa kutoka nchini Japan,na chama katika 
mkoa huo kinaundwa na vilabu mbalimbali ambavyo klabu mama ni Ralway 
club, Pasua Club,  Mwenge Club, Ccp Club,Rau Club,na vilabu vingine 
vinaundwa na wanafunzi mbalimbali ambapo kila club ina zaidi ya 
wanafunzi 20-30.hivyo wanawaomba ,Taasisi mbalimbali 
,wafanyabiashara,makampuni mbalimbali  hata watu binafsi kujitokeza 
kuudhamini mchezo huo wa Karate.
JOCKTAN MALULI, DANIEL MSIRIKALE WAIBUKA WASHINDI KATIKA SHINDANO LA BONGO STYLE
Mshindi
 wa Ubunifu mitindo Jocktan Cosmas Maluli A.k.a Makeke(aliyeshika cheti)
 akiwa katika picha ya pamoja na  waratibu wa shindano hilo kuanzia 
kushoto ni  Zamda George, Comfort Badaru, Martin Kadinda, Reuben Nabora 
na Stanley Kamana. 
Mshindi wa kipengele cha The Best Photographer, Daniel Msirikale (mwenye miwani) akipokea tuzo yake. 
Mratibu wa FASDO nchini, Joyce Msigwa  akitoa muhtasari wa shindano la Bongo Style.
Mshereheshaji, Mario Mpingirwa akifafanua jambo. 
Mtumbuizaji wa ngoma za asili akionesha uwezo wake wa kuchezea nyoka. 
  SHARE 
  









No comments:
Post a Comment