
Misimamo Mikali Ya Vijana Wa Mlimani (1)
- Julius Nyerere Alikoshwa Na Michango Ya Vijana Wasomi Wa Enzi Hizo..
Mwandishi Born Again Pagan ( BAP) Anaandika...
Makala
haya kwanza yaliandikwa kwenye “Kijiji” chetu (mjengwablogspot.com)
mwezi Mei, 2007, chini ya kichwa cha habari, “BAP Anavyomwelezea Yoweri
Museveni”. Madhumuni yake
yalikidhi
ombi la “Mwenyekiti wa Kijiji” kunitaka nitoe maelezo kidogo juu ya
wanafunzi wenzangu Darasa la 1970 hapo Mlimani: Yoweri Kaguta Museveni
na Hirji.
Nilianza
kwa kutoa hoja kwamba haiwezekani kabisa kuweza kusimulia ya Yoweri
Kaguta Museveni na Hirji bila kutoa, pengine, “background” ya miaka kumi
ya kuanzia 1960 na jinsi matukio hayo yalivyojenga mikitadha
iliyozalisha wanafunzi wenye msimamo mkali, kama akina Yoweri Kaguta
Museveni na Hirji.
Katika
makala haya yaliyohaririwa na kuongezea maelezo zaidi (pamoja na
kubadili kichwa chake), ninagusia baadhi ya matukio ya miaka hiyo, na
jinsi yaliyochangia katika kuivisha maisha ya ujana wa akina Yoweri
Kaguta Museveni (Uganda), Hirji, Issa Shivji (Tanzania) pamoja na
wengineo wengi waliomaliza hapo Mlimani mwaka 1970, kwa mfano:
Souma
(Guinea), Archibord Kapote Mwakasungura (Malawi), John Garang (marehemu)
wa Sudani, Salim Msoma, Issa Shivji, Nimrod Mkono, Moses Maira
(marehemu), Ali Mchumo, James Kateka, Augustine Mahiga, Adamu Marwa,
Pius Ngw’andu, Crispin Hauli, (marehemu), Abdallah Ngororo (marehemu),
Patrick Qorro, Jenerali Ulimwengu, na wengine wengi sana,kama mimi.
Vile
vile, makala haya yanachangia juu ya hali hapo Mlimani miaka yetu ya
1966-1970; mkwaruzano baina ya vyama vya wanafunzi vya USARF/TYL na USU
kuhusu suala la “Rag Day”; umoja wa USARF na TYL; makala yanamtoa Hirji
kando kidogo na kuzingatia tu ya Yoweri Kaguta Museveni (kwa makusudi);
na mwisho, mgomo wa Jumamosi, 22 Oktoba, 1966.
Sisemi
kuwa hao waliomaliza mwaka 1970 hapo Mlimani ndio tu maisha yao ya ujana
yaliiva na kuwa na msimamo mkali. La hasha! Wengine walikuwa hawana
msimamo huo! Na walikuwepowengine nyuma yetu wenye msimamo mkali, pia,
ikiwa ni pamoja na hao waliotutangulia. Ila nawataja hao wa mwaka 1970
kwa sababu ndio lilikuwa darasa letu.
Matukio ya Miaka Kumi Kuanzia 1960
Tumetoka
mbali; tunakwenda mbali, pia. Kati yetu (wewe na mimi) huko tuendako
hakuna aliyewahi kupafikia, ingawa tunapanga kuwasili huko. Miaka kumi
ya kuanzia 1960 ilikuwa yamatukio mengi na mikakati mingi, ki-ulimwengu
na ki-taifa (Tanzania). Ufuatao ni mtiririko wa matukio na mikakati
hiyo; lakini si ki-miaka (chronology).
Moja,
misukosuko ya ki-mataifa ya miaka ya kuanzia 1960 ilikuwa ni kupanuka
kwa itikadi eti ya u-Komunisti. Kudhibiti kupanuka kwa u-Komunisti
duniani kuliongozwa na Amerika ikisaidiana na Nchi za Magharibi, mithili
ya hadithi ya kuweka kifuniko jini lisitoke kabisandani ya chupa!
Nchi hizi
ziliuona u-Komunisti kuwa ni utamaduni uliowania kuua ule wa ki-Bepari.
Michakatohiyo ikazua, eti, Vita Baridi! Amerika ilikania kudhibiti (to
contain) kupanuka kwa u-Komunisti huko Asia ya Mashariki ya Mbali,
Amerika ikawania kuishambulia Vietnam.(P.T)
SHARE








No comments:
Post a Comment