Mameya
wawili wa zamani wa nchini Rwanda lwanapandishwa kizimbani katika
mahakama nchini Ufaransa kwa shutuma za makosa ya kibinadamu na
kushiriki mauaji ya halaiki ya mwaka 1994. Octavian Ngenzi na mwenzake
Tito Barahira kwa pamoja wanatuhumiwa kuwa na mchango wa moja kwa moja
katika mauaji hayo.
Kesi hii
ya pili kufunguliwa na mahakama maalum iliyoundwa na Ufaransa kwa ajili
ya kuwashitaki watuhumiwa wa Kinyarwanda waliokimbilia nchini humo,
inatarajiwa kubainisha mwelekeo wa mahusiano baina ya nchi hizo mbili.
Kwa
miongo miwili sasa, Rwanda imekuwa ikiituhumu Ufaransa kwa ushiriki
katika mauaji ambayo yaliwaua raia laki nane, ikisema kuwa Ufaransa
iliisaidia serikali ya wakati huo iliyokuwa ya Kihutu. Miaka miwili
baadaye katika kumbukumbu ya miaka 20 ya mauaji hayo, rais wa nchi hiyo
Paul Kagame aliwatuhumu waziwazi wanajeshi wa Ufaransa sio tu kwa
kusaidia bali kwamba walihusika moja kwa moja katika mauaji hayo.
Na sasa
Octavian Ngenzi na Tito Barahira wanapandishwa kizimbani kwa ushiriki
wao wa moja kwa moja wa kuwaua mamia ya wakimbizi wa Kitutsi waliokuwa
wamejihifadhi katika kanisa mnamo aprili 13 mwaka 1994 huko mashariki
mwa mji wa Kabarondo.(P.T)
SHARE








No comments:
Post a Comment