Maporomoko ya jengo la ghorofa sita la tarehe 29 Aprili yaliwaua watu 49 mjini Nairobi, mji mkuu wa Kenya.
Na RFI
Watu 49
ndio walipoteza maisha wiki moja iliyopita wakati jengo la ghorofa sita
lililopoporomoka katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, polisi ya Kenya
imetangaza Jumapili hii.
Jengo
hili lililojengwa karibu na mkondo wa maji, lilitangazwa na mamlaka
kwamba lilijengwa eneo hatari, bila hata hivyo wamiliki wa jengo hilo
kutojali onyo hilo.
Jengo
hili la ghorofa sita liliporomoka baada mvua kubwa kunyesha usiku wa
Aprili 29 katika kata ya watu wenye maisha duni ya Huruma, mjini
Nairobi.
"Miili
mingine saba ilitolewa katika vifusi vya jengo hilo mwishoni mwa juma
hili", na kupelekea idadi ya watu waliopoteza maisha kuongezeka na
kufikia 49, " Mkuu wa polisi, Yafethi Koome, amesema.
Tukio
hilo la jengo kuporomoka ni la mwisho katika mfululizo wa matukio mabaya
yaliyosababishwa na upanuzi wa haraka wa mji wa Nairobi ambapo
ukiukwaji wa sheria ya mipango miji ni mara chache kuadhibiwa.
Wamiliki wawili wa jengo hili na maafisa watatu wa serikali walihojiwa Jumatano na polisi kabla ya kuachiwa kwa dhamana.(P.T)
SHARE








No comments:
Post a Comment