TRA

TRA

Saturday, October 29, 2016

DAVID MOYES MATATANI KWA KUMUINGILIA MWAMUZI, FA YAMPA MASAA YA KUJITETEA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


_92118214_moyes_getty
Kocha Mkuu wa klabu ya Sunderland ya Uingereza David Moyes ameshtakiwa na chama cha soka cha Uingereza kwa utovu wa nidhamu wakati wa mechi dhidi ya Southampton Jumatano.
Southampton walishinda mechi hiyo ya Kombe EFL Cup uwanjani St Mary’s kupitia bao la Sofiane Boufal na kuwafanya vijana wa Moyes kuyaaga mashindano hayo ambayo yamefikia katika hatua ya robo fainali.
Chama cha Soka cha Uingereza (FA) kimesema kuwa ,Moyes alitumia lugha ya kutusi au maneno ya kuudhi akiyaelekeza kwa mwamuzi wa mechi baada ya timu yake kufungwa.
Kisa hicho kilitokea dakika ya 90 refa Chris Kavanagh alipokataa kuwapa Sunderland penalti baada ya mshambuliaji wa Sunderland Victor Anichebe kuonekana kuchezewa visivyo eneo la hatari na beki wa Southampton huku zikiwa dakika za majeruhi.
Moyes, aliyeteuliwa kuwa Kocha wa Sunderland wanaojulikana kuwa Paka Weusi Julai, ameshinda alama mbili pekee kutoka kwa mechi tisa ligini na wakiwa na kibarua kingumu watakapowaalika washika bunduki Arsenal hapo kesho.
Aidha kwa mujibu wa FA imempa kocha huyu uhuru wa kujieleza na kujitetea hadi saa tisa alasiri kwa saa za Afrika Mashariki Jumanne kujibu tuhuma hizo. (P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger