TRA

TRA

Saturday, August 26, 2017

MASKINI. KIJANA AFARIKI KWA KUKANYAGWA NA TEMBO

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



SeeBait
Kijana Emmanuel Ernest wa kitongoji cha Ilolo, Mvumi Misheni wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma, amefariki dunia baada ya kukanyagwa na tembo huku mwingine akijeruhiwa vibaya baada ya tembo huyo kuvamia mashamba ya zabibu.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema tembo huyo alikuwa akitafuta maji majira ya alfajiri hivyo baadhi ya wanakijiji baada ya kumuona walikusanyika na kupiga mayowe, kitendo kilichomfanya mnyama huyo kukasirika na kuanza kuwafukuza kabla ya kumkuta marehemu Emanuel akiwa na mdogo wake wakichimba mitaro ya mizabibu na kumkanyaga kifuani na kumvunja mbavu nne na kusababisha kifo chake.
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mvumi Misheni, Peter Songoro, amethibitisha kupokea majeruhi wawili, akiwemo marehemu na mdogo wake Amani Joseph ambaye alikanyagwa mgongoni na kisha utumbo kutoka nje, kabla ya Emmanuel kufariki baadaye wakati akipatiwa matibabu.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger