TRA

TRA

Saturday, August 26, 2017

Trump aagiza watu waliobadili jinsia kutoajiriwa

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Rais Donald Trump ameagiza idara ya ulinzi Marekani kusitisha uajiri katika jeshi wa watu waliobadilisha jinsia zao.

Trump aliashiria hatua hiyo ghafla katika ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter mwezi jana.


 Wanaharakati wa watu waliobadili jinsia wakiandamana wakipinga agizo la rais Trump

Katika ilani kwa waziri wa ulinzi Jim Mattis, Trump amesema Pentagon ni lazima irudishe marufuku hiyo.

Idara hiyo ya ulinzi itaamua hatma ya watu ambao wamebadiisha jinsia na ambao tayari wanalitumikia jeshi.

Agizo hilo pia linasitisha nafasi ya wanajeshi wa kiume na wa kike kufanyiwa upasuaji wa kubadili jinsia zao.

CHANZO:BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger