TRA

TRA

Monday, March 28, 2016

Serikali ya Syria yaukomboa tena mji wa Palmyra

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Wanajeshi wa Syria wakiwa na bendera ya nchi hiyo baada ya kuukombowa tena mji wa Palmyra. (27.03.2016)
Wanajeshi wa Syria wakiwa na bendera ya nchi hiyo baada ya kuukombowa tena mji wa Palmyra. (27.03.2016)
Vikosi ya serikali ya Syria vikisaidiwa na mashambulizi ya anga ya Urusi Jumapili (27.03.2016) vimeukombowa tena mji wa kale wa Palmyra uliokuwa ukishikiliwa ma kundi la Dola la Kiislamu tokea mwezi wa Mei.
Vyombo vya habari vya taifa na shirika la uangalizi wa haki za binaamu vimesema mji huo wa kale wa miaka 2,000 ambao ni turathi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu,Sayansi na Utamaduni (UNESCO) uko kwenye mikono ya serikali baada ya mapigano makali yaliyodumu kwa wiki kadhaa.
Duru za kijeshi zimeliambia shirika la habari la Ufaransa (AFP) kwamba "baada ya mapigano makali ya usiku jeshi lina udhibiti kikamilifu mji wa Palmyra ikiwa ni mji wenyewe wa kale na vitongoji vya wakaazi wa mji huo."
Shirika la Uangalizi wa Haki za Binaadamu la Syria limesema milio ya risasi ilikuwa bado ikiendelea kusikika Jumapili katika eneo la mashariki ya mji huo lakini wapiganaji wengi wa kundi la Dola la Kiislamu walikuwa wameondoka kutoka mji huo.(P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger