Kutoka Club Deportive Tenerife Hispania kwenye majaribio ya Farid Musa wa Azam FC
Winga mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania na Azam FC Farid Musa yupo Hispania anaendelea na majaribio yake ya kutafuta nafasi ya kucheza soka la kulipwa, Farid ameendelea na majaribio yake Club Deportive Tenerife ya Hispania.
Farid amethibitisha kuendelea vizuri kiafya lakini ameiambia millardayo.com kuwa ana siku ya nne Club Deportive Tenerife ambapo hapo anakaa wiki moja halafu anaendelea na majaribio katika vilabu vingine vya hapo Hispania alivyotafutiwa na wakala wake John Sorzano.
SHARE
No comments:
Post a Comment