TRA

TRA

Tuesday, April 5, 2016

WAKALA WA UFUNDI NA UMEME(TEMESA) YAZUIA UTENGENEZAJI WA MAGARI YA SERIKALI KIHOLELA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



ngo
Waziri Edwin Ngonyani akimsikiliza Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi. Manase Ole Kujan alipofanya ziara katika idara hiyo hivi karibuni.
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Wakala wa Ufundi na Umeme(TEMESA) imewazuia wamiliki na waendeshaji wa karakana teule zilizopewa mamlaka na TEMESA kutengeneza magari na vifaa vya Serikali  kutofanya matengenezo ya magari na vifaa hivyo bila kufata utaratibu wa wakala.
Akizungumza katika kikao kati ya TEMESA, wamiliki na waendeshaji wa karakana teule, Kaimu Mtendaji Mkuu wa TEMESA,  Mhandisi Manase Lekujan amesema karakana teule zinatakiwa kufata taratibu husika katika kufanya matengenezo ya magari na vifaa vya Serikali.
“Tumeitisha kikao hiki na wamiliki wa karakana teule tunazofanya nazo kazi ili tukumbushane kuhusu kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizopo kwenye mikataba yetu, katika kuweka mpango mzuri wa kuwa na taarifa sahihi za matengenezo ya magari na vifaa vya Serikali katika karakana zetu ili kuondokana na changamoto zilizopo na kuongeza ufanisi wa kazi zetu” Alisema Mhandisi Manase.
Akifafanua kuhusu Sheria ya Manunuzi ya mwaka 2011, Mwanasheria wa TEMESA, Gratian Mali amesema sheria inatoa nafasi kwa Wakala wa Ufundi na Umeme kutafuta karakana binafsi kusaidia shughuli za matengenezo ya magari na vifaa vya Serikali pale ambapo karakana  za Serikali zinapokuwa na kazi nyingi au kukosa baadhi ya vifaa kwa ajili ya matengenezo na kazi hizo hutolewa kwa vibali maalumu kutoka TEMESA.
Akizungumza mara baada ya kikao na TEMESA mmoja wa wamiliki wa karakana ya Nduvin Auto Works, Al Haj Masoud Msangi amesema kikao hicho kimekuwa cha mafanikio kwani imefika wakati kwa karakana teule kutekeleza agizo la kutengeneza magari na vifaa vya Serikali kwa kufata Sheria na taratibu zilizopo na sio kufanya shughuli zake kiholela.
TEMESA imeanzishwa chini ya Sheria ya Wakala Na 30 ya mwaka 1997 na ilizinduliwa rasmi Juni 23 mwaka 2006 na ina kazi ya kufanya matengenezo ya magari na vifaa vya Serikali,kusimamia huduma za vivuko na usimikaji na matengenezo ya mifumo ya umeme na eletroniki. (P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger