Kikundi
cha TYT kikitoa burudani wakati uzinduzi wa promosheni ya Million 100
na Tusker Fanya Kweli Uwini kanda ya ziwa uliofanyika jijini Mwanza
-Cross Park Bar Igoma.
Baadhi
ya wafanyakazi wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Kanda ya Ziwa wakicheza
kufurahia uzinduzi wa Tusker Fanya Kweli Uwini jijini Mwanza.
Meneja
Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Kanda ya Ziwa Patrick Kisaka
akitoa maelezo ya promosheni hiyo kabla ya kuzindua rasmi wakati wa
hafla fupi ya uzinduzi wa promosheni ya Million 100 na tusker Fanya
Kweli Uwini, iliyoandaliwa na kampuni hiyo jijini Mwanza.
Baada ya kutikisa jiji la Dar es Salaam
na manispaa ya Moshi leo Kampuni ya Bia ya Serengeti imeendelea kuwapa
raha wateja wake kwa kuzindua promosheni ya Milioni 100 na Tusker- Fanya
Kweli na Uwini Kanda ya ziwa ambapo Millioni 100 za Tusker Lager
kushindaniwa.
Uzinduzi
huo uliofanyika jijini Mwanza Katika Bar ya Cross Park iliyopo Igoma
wilayani Ilemela, ulipambwa na maonyesho ya barabarani ambapo msafara
ulianzia Kiwanda cha Serengeti Igoma na kuishia Cross Pack Bar huku
ukipokelewa na shamrashamra za aina mbalimbali.
Promosheni
hiyo itawapa fursa wateja kujishindia pesa taslimu Milioni 1 kwa
washindi kumi (10) kila wiki kwa muda wa wiki kumi na kufanya jumla ya
Milioni mia kushindaniwa na Zawadi za bia kibao. Promosheni hii
ilizinduliwa rasmi na itaendeshwa kwa muda wa wiki kumi. Uzinduzi huo
ulihudhuriwa na wadau mbalimbali wa Kampuni hiyo pamoja na wana habari.
Hii
si mara ya kwanza kwa Kampuni ya Bia ya Serengeti kuendesha promosheni
kama hii kwani ni wengi wameshanufaika kupitia promosheni mbalimbali za
mfumo huu na hata kubadili maisha ya watumiaji wa bidhaa zake kwa kiasi
kikubwa. Kupitia bia ya Tusker Lager Kampuni hiyo inaendeleza kile
kilichokuwepo cha kurudisha fadhila na kutoa shukrani kwa watumiaji wa
bia ya Tusker Lager.
Wateja
wanaweza kujaribu mara nyingi kadiri wawezavyo. Ili kuwa mshindi wa
Tusker milionea, washiriki wataingizwa moja kwa moja kwenye droo
kutokana na vocha walizojaza mahali walipopatiwa huduma na wataweza
kujishindia pesa taslimu na droo hizo zitachezeshwa kila wiki.
Mtumiaji
anapofungua bia ya Tusker Lager (500ml) chini ya kizibo anaweza kupata
kizibo cha ‘Tusker Milionea’ hii itamuingiza katika droo ya kupata
Milioni moja, au anaweza kupata ‘Bia ya Bure’ – hii inampa mteja bia ya
Tusker papo hapo alipohudumiwa na ikiwa atapata ‘Jaribu tena’ utaendelea
kuburudika kistaarabu ili kuongeza nafasi yako kuibuka mshindi.
Promosheni hii itasimamiwa na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini ili
kuleta ufanisi zaidi.
Akiongea
wakati wa uzinduzi huo jijini Mwanza Meneja Mauzo wa Kanda ya ziwa wa
Kampuni ya Bia ya Serengeti Patrick Kisaka, aliwashukuru wageni wote kwa
kuja kuwaunga mkono na kusema kuwa uzinduzi wa promosheni hiyo ni muendelezo wa kile kilichoanza wiki mbili zilizopita ikiwa ni kutoa shukrani kwa wateja wao kwa kusapoti bidhaa zao.
Alisema
“kuendesha promosheni hii ni kurudisha shukrani kwa wajeta wetu kwa
kutuunga mkono na kusapoti bidhaa zetu, ambapo tunampa mteja sehemu ya
faida tuliyopata Katika mauzo yetu hivyo kuwapa wateja wetu wigo mpana
wa kujiinua kimaisha. Kupitia bia yetu ya Tusker Lager tunampa fursa
mnywaji na mdau wa bia hii kufanya kweli hivyo watumiaji wa bia ya
Tusker wanaweza kujishindia shilingi Millioni moja kwa washindi kumi kwa
muda wa wiki kumi ambao tutawapata kutokana na droo tutakazochezesha
kila wiki.”
Naye
‘Commercial Planning & Activations Manager’ wa Kampuni ya Bia ya
Serengeti Denis Tairo alisema “Kanda ya ziwa ni sehemu muhimu sana kwa
soko letu, wadau wa jiji hili la Mwanza mmekua mstari wa mbele na haikua
rahisi sisi kufika hapa leo bila ninyi wadau wetu basi nasi tunasema
burudika na bia ya Tusker ili upate nafasi ya kushiriki katika
promosheni hii, haijalishi upo wapi na unafanya nini lakini amini kuwa
kila wiki ni Millioni kumi zinatolewa kwa watumiaji kumi wa bia ya
Tusker.”
Wapenzi
na wadau wa Tusker wataweza kushuhudia droo za Promosheni ya Milioni
100 na Tusker zitakazofanyika kila wiki siku ya ijumaa na kurushwa moja
kwa moja katika runinga. Washindi
watakaopatikana watakabidhiwa pesa zao ambazo watazipokea kwa njia ya
mtandao kila ijumaa inayofuatia kwenye hafla maalum ya makabidhiano.
Milioni 100 na Tusker Fanya kweli na Uwini itadumu kwa muda wa wiki kumi
nchi nzima.
SHARE
No comments:
Post a Comment