TRA

TRA

Thursday, June 30, 2016

Magazeti ya Leo

No comments:


Kampuni ya Nation yafunga vituo vyake

No comments:


Jumba na Nation mjini Nairobi
Kampuni kubwa zaidi ya Habari Afrika mashariki, Nation Media Group, imeamua kufunga baadhi ya vituo vyake.
Hatua hiyo itashuhudia idadi kubwa zaidi ya watu kupoteza kazi zao.
Katika taarifa iliyopokelewa nchini Kenya, NMG kama inavyofahamika, imeamua kufunga vituo kadhaa vya Radio kama vile Nation FM, QFM na KFM iliyoko Kigali nchini Rwanda.
Mbali na vituo hivyo vya Radio, itafunga pia kituo chake kimoja cha Runinga QTV.
Nation Media Group inasema sasa itaelekeza juhudi zake kuboresha taarifa za mitandaoni.
Kampuni hiyo ilianzishwa na muathama Aga Khan yapata miaka sitini iliyopita.BBC

Tishio la Dola la Kiislamu lainyemelea Kenya

No comments:


Imebainika kwamba kwamba ushawishi wa kundi la Dola la Kiislamu Afrika Mashariki umeongezeka kwa kuwaandikisha vijana wa Kenya kuendesha mapambano ya jihadi nchi za nje na baadhi yao kurudi Kenya kuitishia nchi hiyo.
Mashirika ya ujasusi nchini Kenya yanakadiria kwamba takriban wanaume na wanawake 100 yumkini wakawa wamekwenda kujiunga na kundi la Dola la Kiislamu nchini Libya na Syria na kuzusha wasi wasi kwamba baadhi yao huenda wakarudi nchini humo kufanya mashambulizi kwa Kenya na katika vituo vya kigeni, katika nchi ambayo tayari ni muhanga wa mashambulizi ya kigaidi yanayofanyika kila mara nchini humo.
Rashid Abdi mchambuzi mwandamizi katika Shirika la Kimataifa la Kushughulikia Mizozo ambalo ni jopo la ushauri lilioko katika mji mkuu wa Kenya Nairobi amesema "kwamba hivi sasa kuna tishio la kweli linaloikabili Kenya kutoka kundi la Dola la Kiislamu na hatari hiyo itazidi kuongezeka."
Tatizo la wafuasi wa itikadi kali ambao mara nyingi ni watu wenye shauku lakini wasiokuwa na mafunzo, kupatiwa mafunzo stadi ya kigaidi na kundi la Dola la Kiislamu na kurudi nyumbani kufanya mashambulizi ni tatizo ambalo tayari mataifa ya Ulaya yanakabiliana nalo na yumkini hivi karibuni likawa pia ni tatizo kwa Kenya.
Mshauri elekezi wa masuala ya usalama na afisa polisi wa zamani George Musamali ameliita hilo kuwa ni "bomu linasubiri kuripuka."Amesema watu kwenda Libya au Syria sio tatizo kwa Kenya tatizo ni kile watakachokifanya wakati watakaporudi.
Mashambulizi ya kigaidi sio tu kigeni Kenya
Shambulio la kwanza la kigaidi la Al- Qaeda nchini Kenya ilikuwa ni kuripuliwa kwa ubalozi wa Marekani hapo mwaka 1998 na hivi karibuni kabisa yalikuwa ni mauaji katika chuo kikuu cha Garissa mwaka jana lakini tishio la Dola la Kiislamu ni jipya na bado kueleweka vyema.
Hapo mwezi wa Machi wanaume wanne walifikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutaka kwenda Libya kuijunga na kundi la Dola la Kiislamu.
Baadae hapo mwezi wa Mei polisi ya Kenya ilitangaza kukamatwa kwa mwanafunzi wa udaktari,mke wake na shoga yake wanaotuhumiwa kuwaandikisha watu kujiunga na kundi la Dola la Kiislamu na kupanga shambulio la kibiolojia kwa kutumia anthrax.
Inasemekana wanafunzi wengine wawili wa udaktari wamekimbia.
Kukamatwa kwa silaha
Wiki tatu baadae polisi ya Kenya ilitangaza kukamatwa kwa wanachama wengine wawili wa mtandao wa kundi la Dola la Kiislamu ambao ulikuwa ukitaka kujipenyeza Kenya ili kuweza kufanya mashambulizi ya kigaidi dhidi ya Wakenya wasiokuwa na hatia.
Polisi ilisema imegunduwa vitu ambayo hutumiwa na magaidi kutengeneza mabomu ya kienyeji pamoja na mikuki na mishale iliotiwa sumu.
Wakati baadhi ya wataalamu wanatupilia mbali ishara ya shambulio kubwa lainyemelea Kenya wanakiri kwamba kuna tishio la dhati la kundi la Dola la Kiislamu kupandikiza itikadi kali,kuandikisha watu kujiunga nalo na baadae kuwarudisha nyumbani.DW

MAJALIWA AKUTANA NA WAJUMBE WA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

No comments:


C1
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva   katika mazungumzo kati yake na wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi  yaliyofanyika kwenye  makazi yake mjini Dodoma Juni 30, 2016.
C2
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  akimsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva katika mazungumzo kati yake ya Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi yaliyofanyika  kwenye makazi yake mjini Dodoma Juni 30, 2016.
C3
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva Taarifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa 2015 kwenye makazi yake mjini Dodoma Juni30, 2016.
C4
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wajumbe wa Tume ya taifa ya Uchaguzi kwenye Makazi yake  mjini Dodoma Juni 30, 2016. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Damian Lubuva.
C5
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi baada ya kuzungumza nao kwenye makazi yake mjini Dodoma Juni 30, 2016. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Damiana Lubuva.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)(P.T)

Dkt. Mahiga akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda

No comments:


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe.Loiuse Mushikiwabo, alipomtembelea leo katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika kuimarisha na kuboresha mahusiano yaliyopo baina ya nchi hizo mbili, pamoja na Ziara ya Rais wa Jamhuri ya Rwanda Mhe. Paul Kagame anayetarajiwa kuwasili nchini kesho kwa ziara ya siku mbili. 
Kaimu Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. James Bwana alipokuwa akimkaribisha Mhe. Waziri Mushikiwabo mara baada ya kuwasili Wizarani. 
Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Samuel Shelukindo, akiwa na Kaimu Mkuu wa Itifaki, Bw. James Bwana na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Medard Ngaiza wakifuatilia mazungumzo.
Balozi wa Jamhuri ya Rwanda nchini, Mhe. Eugene Kayihura (kulia) pamoja na Afisa aliyeambatana na Mhe. Waziri Mushikiwabo wakifuatilia mazungumzo.
Wakati mazungumzo yakiendelea.
Wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo.

Wawekezaji wazawa wana haki kuwekeza kwenye gesi, mafuta

No comments:


Na Greyson Mwase

Serikali imesema wawekezaji wazawa wana haki ya kuwekeza kwenye sekta za mafuta na gesi ili sekta hizo ziwe na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi.

Hayo yamesemwa na mtaalam kutoka Idara ya Nishati, Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Petro Marwa kwenye maonesho ya kimataifa ya sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Mhandisi Petro alisema kumekuwepo na dhana kuwa wawekezaji kutoka nje ya nchi wanapewa kipaumbele katika uwekezaji kwenye gesi na mafuta jambo ambalo si sahihi.

Alisema ili kuhakikisha kuwa kila mtanzania ananufaika na uwekezaji kwenye sekta za gesi na mafuta, Serikali imeweka sheria nzuri za kuwezesha watanzania kuwa sehemu ya uchumi wa gesi na mafuta.

“ Kwa mfano Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015 kifungu cha 218 kinaeleza ushiriki wa serikali kupitia Kampuni ya Mafuta ya Taifa (National Oil Company) na kifungu cha 219 na 220 kinaainisha ushiriki wa watanzania katika utoaji wa huduma na bidhaa kwa makampuni yaliyowekeza nchini kwenye sekta za mafuta na gesi,” alisema Mhandisi Petro.

Mhandisi Petro aliendelea kusema kuwa serikali imeweka mikakati mbalimbali kuhakikisha watanzania wanakuwa si watazamaji kwenye uvunaji wa rasilimali za gesi na mafuta bali wanakuwa ni washiriki kamili na kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa nchi.

Akielezea mikakati hiyo, Mhandisi Petro alisema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini ilianzisha kozi mbalimbali zinazohusu mafuta na gesi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Chuo cha Madini (MRI).

Aliongeza kuwa Wizara imekuwa ikiwezesha wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo ya sayansi kupata ufadhili wa kusomea masuala ya mafuta na gesi katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Mhandisi Petro alitoa wito kwa watanzania wote kuchangamkia fursa zilizopo katika sekta za mafuta na gesi ili nchi iweze kutoka kwenye kundi la nchi masikini duniani na kuingia katika orodha ya nchi zenye kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 kama Dira ya Maendeleo ya Taifa inavyofafanua.
Afisa Habari, Mhandisi Yisambi Shiwa (kulia) kutoka Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA) akielezea madini ya dhahabu yanavyochenjuliwa kwa mteja aliyeshika sampuni ya madini hayo kwenye banda la TMAA katika maonesho hayo.
Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Phillip Mathayo (kushoto) akielezea majukumu ya Wizara kwa mteja aliyetembelea banda hilo katika Maonesho ya Kimataifa ya Saba Saba (Dar es Salaam International Trade Fair) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Washiriki kutoka Kampuni ya Kuendeleza Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC) wakiwa katika picha ya pamoja kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Saba Saba (Dar es Salaam International Trade Fair) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa wateja (kushoto) akitoa maoni yake kwenye banda la Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Saba Saba (Dar es Salaam International Trade Fair) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Washiriki kutoka Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) wakiwa katika picha ya pamoja kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Saba Saba (Dar es Salaam International Trade Fair) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Neema Mwambenja kutoka Taasisi ya Environmental Foundation for Tanzania (EFFORT) ambayo ni mdau wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) (katikati) akitoa maelezo ya shughuli zinazofanywa na taasisi hiyo kwenye banda la REA, kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Saba Saba (Dar es Salaam International Trade Fair) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Odriana Magige kutoka taasisi hiyo.
Mhandisi Migodi kutoka Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Suleiman Khalid (katikati) akielezea shughuli zinazofanywa na shirika hilo. Kushoto ni Afisa Usalama na Mazingira kutoka shirika hilo Paul Thobias.
Banda la Wizara ya Nishati na Madini na Tasisi zake kama linavyoonekana pichani kwenye kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Saba Saba (Dar es Salaam International Trade Fair) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Afisa Habari, Mhandisi Yisambi Shiwa (kushoto) na Mkaguzi wa Madini Mwandamizi Jeremiah Hango (kulia) kutoka Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA), wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kuwahudumia wateja katika Maonesho ya Kimataifa ya Saba Saba (Dar es Salaam International Trade Fair) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Wednesday, June 29, 2016

Magazeti ya Leo

No comments:


 

Shambulio katika uwanja wa ndege lauwa watu 41 Istanbul

No comments:


Washambuliaji wa kujitowa muhanga wamewauwa zaidi ya watu 41 na kujeruhi wengine 140 katika shambulio dhidi ya uwanja wa ndege wa Ataturk mjini Istanbul katika mfululizo wa miripuko ya mabomu dhidi ya Uturuki.
Idadi ya watu waliouwawa katika shambulio la uwanja wa ndege wa Istanbul imeongezeka na kufikia 41. Awali Waziri Mkuu wa Uturuki Binali Yidirm amesema watu 36 wameuwawa hapo jana wakiwemo washambuliaji watatu wa kujitowa muhanga ambao waliwasili katika uwanja wa ndege huo kwa kutumia taxi na kujiripuwa mara tu baada ya kuanza kufyatuwa risasi.Waziri wa sheria wa Uturuki Bekir Bozdag amesema watu 147 wamejeruhiwa.
Akizungumza na waandishi wa habari katika uwanja wa ndege huo baada ya kutokea kwa shambulio hilo hapo jana Waziri Mkuu wa Uturuki Binali Yidrim amesema kundi la Dola la Kiislamu linaonekana kuhusika na shambulio hiilo
Binali amesema "Uchunguzi wa vikosi vyetu vya usalama unaashiria kwamba shambulio hilo la kigaidi limetekelezwa na kundi la Daesh na licha ya kwamba uchunguzi unakielekezea kidole kundi hilo la Dola la Kiislamu uchunguzi huo bado unaendelea.Uwanja wa ndege unafunguliwa tena kwa safari saa nane usiku na safari za ndege zitarudi katika hali ya kawaida."
Kwa mujibu wa maafisa polisi ilifyatuwa risasi kujaribu kuwazuwiya washambuliaji wawili kabla hawajafika kituo cha ukaguzi wa usalama katika ukumbi wa kuwasili abiria katika uwanja wa ndege huo lakini waliripuwa mabomu yao. Afisa wa Uturuki amesema wengi waliouwawa walikuwa ni raia wa Uturuki lakini pia kuna wageni miongoni mwa watu waliouwawa.
Shambulio lafanana na la Brussels
Shambulio hilo kwa kiasi fulani linafanana na shambulio la kujitowa muhanga lililofanywa na wanamgambo wa kundi la Dola la Kiislamu katika uwanja wa ndege wa Brussels hapo mwezi wa Machi na kuuwa watu 16 kabla ya shambulio jengine kuuwa watu wengine 16 siku hiyo hiyo katika njia ya reli ya chini ya ardhi katika mji mkuu huo wa Ubelgiji.
Mashahidi walirepoti kusikia milio ya risasi kutoka sehemu mbali za uwanja wa ndege huo wa Atartuk ambao ndio uwanja wa ndege mkubwa kabisa nchini Uturuki na wa tatu kwa kuwa na harakati kubwa za safari za kimataifa barani Ulaya.
Rais Recep Tayyip Erdogan amelani shambulio hilo la kigaidi dhidi ya raia wasiokuwa na hatia.
Uwanja wafunguliwa tena
Ndege tayari zimeanza kutuwa tena katika uwanja wa ndege huo leo ajafiri baada ya uwanja wa ndege huo kufungwa kabisa kwa masaa kadhaa hapo jana kufuatia shambulio hilo la kigaidi.Mamia ya safari zilifutwa kufuatia shambulio hilo.
Shirika la ndege la Uturuki ambalo limefuta zaidi ya safari 340 limekuwa likiwarejeshea abiria fedha zao au tiketi mbadala lakini bado kuna mkanganyiko kwa wasafiri wengi.
Shambulio hilo la jana ni baya kabisa kuwahi kushuhudiwa nchini humo kwa zaidi ya muongo mmoja mjini Istanbul.Kundi la Dola la Kiislamu limekuwa likilaumiwa kwa kuhusika na mashambulio kadhaa nchini Uturuki katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.DW

LAPF NDANI YA MAONESHO YA SABASABA 2016

No comments:


L
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF Bw. James Mlowe akizungumza na waandishi wa habari kuhusu sababu za ushiriki wa Mfuko katika maonyesho ya biashara ya kimataifa (Saba Saba 2016).
L2
Afisa Mifumo ya kompyuta kutoka Mfuko wa Pensheni wa LAPF Bw. Yohana Nyabili akitoa maelezo kwa mwanachama wa Mfuko pamoja na kumpatia taarifa ya michango yake mara baada ya mwanachama huyo kutembelea banda ya Mfuko kwenye maonyesho ya biashara ya kimataifa (Saba Saba 2016).(P.T)

PBZ YAADHIMISHA SHEREHE ZA MIAKA 50 KWA KUSAIDIA JAMII NA KUTEMBELEA HOSPITALI YA KIDONGOCHEKUNDU.

No comments:



Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akimkabidhi msaada wa magodoro 100 Kamishna Msaidizi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar Omar Salum Mgaza. hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Mafunzo Kilimani Zanzibar.
Baadhi ya magodoro 100 yaliotolewa msaada na PBZ kwa ajili ya matumishi ya Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar, ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar. hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Chuo cha Mafunzo Kilimani Zanzibar.  

Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ akizungumza na Maofisa wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar wakati wa kikabidhi msaada wa magodoro kwa ajili ya Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Mafunzo Kilimani Zanzibar.
Kamishna Msaidizi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar Omar Salum Mgaza akitowa shukrani kwa PBZ  kwa msaada wao huo wa magodoro umeletwa wakati muafaka na kuwata taasisin nyengine kujitokeza kutoa misaada.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg.Juma Ameir akisalimiana na Muuguzi Dhamana wa Hospitali ya Kidongochekundu Zanzibar Ndg. Haji Vuai Hilal, wakati walipofika katika hospitali hiyo ya Mental kutowa misaada ya mashuka 200 kwa ajili ya hospitali hiyo. katikatika Afisa Masoko wa PBZ Ndg. Mohammed Nuhu. 
Afisa Masoko wa PBZ Ndg Mohammed Nuhu akisalimiana na Muuguzi Dhamana wa Hospitali ya Mental Kidongochekundu Zanzibar Haji Vuai Hilal. 
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Juma Ameir akizungumza na Uongozi wa Hospital ya Mental Kidongochekundu Zanzibar wakati wa kutembelea hospitali hiyo na kutoa msaada wa mashuka 200 ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya hospitali hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akikabodhi msaada wa mashuka kwa ajili ya hospitali ya Mental Kidogochekundu Zanzibar akipokea msaada huo Muuguzi Dhamani wa hospitali hiyo Ndg Haji Vuai Hilal. ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ kushaidia jamii Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akikabodhi msaada wa mashuka kwa ajili ya hospitali ya Mental Kidogochekundu Zanzibar akipokea msaada huo Muuguzi Dhamani wa hospitali hiyo Ndg Haji Vuai Hilal. ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ kushaidia jamii Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg. Juma Ameir akimkabidhi mmoja wa mgonjwa katika hospitali hiyo Bi Amina Mwinyi msaada wa tende kwa ajili yao katika kipindi hichi cha mfungo wa mwezi wa ramadhani.
Mmmoja wa mgonjwa katika hospitali Bi Amina Mwinyi, hiyo akitowa shukrani kwa niaba ya wezake kwa uongozi wa PBZ kwa msaada wao huo kwao na kuuthamini na kuwataka na Wananchi wengi kujitokeza kuwasaidia kwa vitu mbalimbali.  
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg. Juma Ameir akikabidhi msaada wa tenda mmoja wa wagonjwa wa hospitali hiyo Ndg. Mrisho Idrisa Hussein.

Muuguzi Dhamana wa Hospitali ya Mental Kidongochekundu Zanzibar Ndg Omar Vuai Hilal akitowa shukrani kwa Uongozi wa PBZ na Wafanyakazi wao kwa msaada wao huo katika hospitali hiyo.
Wafanyakazi wa PBZ wakijumuika na Mkurugenzi Mtenda wa PBZ Ndg Juma Ameir katika kutoa huduma kwa wateja ikiwa ni shamrashamra za kuadhimisha miaka 50 ya PBZ tangu kuazishwa kwa benki hiyo wakiwa katika Tawi la Malindi Zanzibar. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar Ndg Juma Ameir akitowa huduma kwa Wateja wa PBZ katika tawi la PBZ Malindi, Pbz imetimisha miaka 50 tangu kuazishwa kwa kwake Zanzibar. 
Wateja wa PBZ wakipita huduma za Kibenki katika Tawi la PBZ Malindi Zanzibar. 
Meneja wa Benki ya Watu wa Zanzibar Tawi la Malindi akitowa huduma kwa wateja wao akiwa na Afisi wa PBZ wakati wa shamrashamra za kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akitowa zawadi kwa Wateja wa PBZ ikiwa ni shamrashamra za kusherehekea miaka 50 ya PBZ kuazisha kutowa huduma za Kibenki Zanzibar.
Wateja wa PBZ wakiwa katika Tawi la Malindi Zanzibar wakisubiri kupata huduma za Kibenki katika tawi hilo.  
Wateja wakipatya huduma katika Benki hiyo Tawi la Malindi Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ akitowa zawadi kwa wateja wa PBZ Tawi la Malindi Zanzibar.
Mteja wa PBZ Zanzibar akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na huduma za Kibenki, wakati wa shamrashamra hizo za kusherehekea miaka 50 ya PBZ na kuwataka kuboresha zaidi huduma zao kwa wateja.

Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ akizungumza na waandishi wa habari malengo na changamoto za PBZ kwa wateja wake na malengo yao kutowa huduma kwa Wateja wao na kuboresha zaidi huduma zao. 
Afisa wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar Ndg Jaha akitowa huduma za kibenki kwa Wateja wao katika tawi hilo PBZ inatimiza miaka 50 tangu kuazishwa kwake. 
Afisa Manunuzi wa PBZ  Bi Mwanaidi Ramadhani akitowa huduma za Kibenki kwa Wateja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar, Maofisa wa PBZ wameungana na wafanyakazi wa Matawi la PBZ kutowa Huduma za Kibenki kuadhimisha miaka 50 ya PBZ tangu kuazishwa kwake.  
Meneja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar akitowa huduma za Kibenki kwa Wateja wa PBZ ikiwa ni shamrashamra za kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar.
Meneja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar akizungumza na waandishi wa habari wakati wa shamrashamra za kutimia miaka 50 ya PBZ Zanzibar.
Afisa manunuzi wa PBZ Bi Mwanaidi Ramadhani akitoa zawadi kwa Wateja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar ikiwa ni kuadhimisha miaka 50 ya PBZ tangu kuazishwa kwake mwaka 1966-2016
Mteja wa PBZ akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na huduma za PBZ ni nzuri na kuwataka kuziboresha zaidi katika kipindi kijacho kwa wateja wao na kuwataka kuongeza huduma na ATM na kuziboresha zaidi huduma hizo kuwafikia hadi wananchi wa vijiji kupata huduma hii ya ATM huko mashamba.

Imetayarishwa na OthmanMapara. 
Zanzinews.com
 
 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger