Kuelekea
mchezo wa watani wa jadi katika jiji la London nchini England maarufu
kama dabi ya London ya Kaskazini kati ya Arsenal watakaowakaribisha
Tottenham Hotspurs katika uwanja wa Emirates siku ya Jumapili, wenyeji
wa mchezo huo wamepata ahueni baada ya wachezaji wake wanne wa kikosi
cha kwanza ambao walikuwa majeruhi kupata nafuu ya majeraha yao mna
kwamba sasa wanaweza kujumuishwa katika katika kikosi kitachocheza
mchezo huo.
Kwa
mujibu wa taarifa zilizopatikana leo zinaonyesha kuwa Theo Walcot, Sant
Carzola, Hector Bellarin na Nacho Monreal ambao wote walikosekana katika
mchezo uliopita wa ligi ya mabingwa barani ulaya dhidi ya Ludogorets
Razgrad mbapo Arsenal walishinda kwa magoli 3-2 wakitokea nyuma baada ya
kutanguliwa kwa mabao 2, wanarejea baada ya kuonekana afya zao
zikiimarika.
Arsenal
wamepoteza mchezo mmoja pekee toka ligi kuu ilipoanza baada ya kupoteza
4-3 dhidi ya Liverpool katika mechi yao ya ufunguzi wa ligi, na baadae
kutoka sare na mabingwa watetezi Leicester City na timu ya Midlesbrough
huku wakishinda mecchi zilizobaki na kufikisha pointi 23 pamoja na
viongozi wengine wa ligi Manchester City na Liverpool.
Mechi
ijayo ni muhimu kwa pande zote mbili kwa kuwa ni mechi ya watani wa jadi
lakini pia ni mechi inayowapa nafasi kujiimarisha kwenye msimamo wa
ligi nchini England. Timu zote zinaonekana kufanya vizuri katika michezo
yao na wachezaji wa Arsenal wanaorejea wamekuwa chachu ya kufanya
vizuri kwa klabu yao ya Arsenal.(P.T)
SHARE
No comments:
Post a Comment