Chanzo Mo Blog
Hatimaye
ile ndoto ya mashabiki wa klabu ya Simba kuona klabu yao ikibadili
mfumo unaotumika sasa wa wanachama ndiyo kuwa wamiliki wa klabu na
kuingia katika mfumo wa kampuni imekamilika.
Hilo
limethibitishwa na Rais wa Simba, Evans Aveva katika mkutano mkuu wa
Simba ambao ulikuwa unafunga msimu wa 2015/2016 kwa kutolewa taarifa na
kuweka mipango mipya kwa msimu ujao.
Hatua
hiyo imekuja baada ya mmoja wa mashabiki wa Simba na Mkurugenzi Mtendaji
na Rais wa makampuni ya Mohammed Enterprises, Mohammed Dewji “MO”
kutangaza nia ya kutaka kununua hisa za asilimia 51 na kutoa Bilioni 20
kwa ajili ya kuisaidia Simba kurudi katika makali yake ikiwa ni pamoja
na kusajili wachezaji wazuri, kocha mzuri, kujenga kiwanja, kuweka vituo
vya kukuzia vipaji vya Simba na vingine vingi.
Kutokana
na jambo hilo, mashabiki wa Simba walionekana kuvutiwa na mipango ya MO
na hivyo kuandamana katika ofisi za klabu na kushinikiza uongozi
kukubaliana na MO ili kununua hisa na kuanza kuwekeza ili Simba irudi
katika makali ya kushinda mataji.
Ipo hapa video ikimuonyesha Rais wa Simba, Evans Aveva akitangaza mkutano wa Simba kuridhia kufanya mabadiliko.
SHARE
No comments:
Post a Comment