TRA

TRA

Thursday, August 18, 2016

Sudan Kusini yakanusha kuwepo kwa mapigano mapya jijini Juba

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


media
Makamu wa kwanza wa rais wa Sudan Kusini Thaban Deng Gai (Kushoto) akisalimiana na rais Uhuru Kenyatta (Kulia) katika Ikulu ya rais jijini Nairobi Agosti 16 2016
Makamu wa kwanza wa rais wa Sudan Kusini Thaban Deng Gai ambaye amekuwa ziarani nchini Kenya, amekanusha ripoti za kuwepo kwa mapigano ya mara kwa mara jijini Juba au karibu na jiji hilo.
Gai ambaye aliteuliwa na rais Salva Kiir mwezi uliopita kuchukua nafasi ya Riek Machar, ameongeza kuwa mapigano ambayo yamekuwa yakiendelea katika jimbo la Upper Nile na mji wa Wau yamesitishwa na kuna amani kwa sasa.
Hata hivyo, amesema kama kuna mapigano yoyote, yanaendelea katika katika jimbo la Equitorial Magharibi karibu na mpaka wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, lakini kwa kiasi kikubwa nchi hiyo ina amani.
Makamu huyo wa kwanza wa rais, alikutana na rais Uhuru Kenyatta siku ya Jumanne, kujadiliana na kuhusu hatua iliyopigwa baada ya mazungumzo ya viongozi wa Afrika Mashariki IGAD kuhusu hali ya usalama nchini humo.

Ujumbe wa Sudan Kusini na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi Agosti tarehe 16 2016
Ni ziara iliyokuja baada ya Sudan Kusini kukubali azimio la Umoja wa Mataifa la kutuma kikosi cha wanajeshi 4,000 kutoka Kenya, Ethiopia na Rwanda kulinda amani na kuzuia mapigano jijini Juba, baada ya machafuko mpya kuzuka mwezi uliopita.
Gai ambaye alikuwa mshirika wa karibu wa Riek Machar, aliongoza ujumbe wa waasi kufanikisha mazungumzo ya amani mwaka uliopita, amesisitiza kuwa alikubali nafasi hiyo kwa sababu wanasiasa wa upinzani wanahitaji amani ya kudumu.
Machar, ambaye hajulikana alipo baada ya kuondoka Juba mwezi uliopita, amepinga kuteuliwa kwa Gai na kusema yeye ndiye Makamu wa kwanza wa rais na rais Kiiir hana mamlaka ya kumteua.RFI

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger