TRA

TRA

Sunday, August 21, 2016

Usain Bolt ashinda dhahabu yake ya tatu Rio

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Shindano la Bolt la mwisho lilikuwa la mita 100 kupokezana vijiti mara nne
Shindano la Bolt la mwisho lilikuwa la mita 100 kupokezana vijiti mara nne
Mwanariadha wa kasi zaidi duniani mzaliwa na Jamaica Usain Bolt amepata dhahabu katika mbio tatu tofauti katike kile kinachojulikana katika kiingereza kama "trible trible" au tatu tatu.
Shindano lake la mwisho lilikuwa la mita 100 kupokezana vijiti mara nne.
Alipokea kijiti mwisho katika timu yake na akafululiza kishujaa na kumshinda mpinzani wake wa karibu kutoka Japan, aliyeshinda Marekani na kuchukua Shaba.
Bolt ameshinda dhahabu mara tatu katika Olimpiki zote tatu alizoshiriki ndipo ushindi wake huu ukatambuliwa kama trible trible yaani tatu tatu.
Ushindi wa Usain Bolt unakuja siku tatu kabla ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa
Ushindi wa Usain Bolt unakuja siku tatu kabla ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa
Bolt mwenye umri wa miaka 29, alishinda dhahabu katika mbio za mita 100 na 200 mjini Rio na ndiye mwanariadha wa kwanza kushinda mbio tatu katika mashindano matatu ya olimpiki
Awali timu ya marekani ya wanawake ilishinda mbio sawa na hizo za kupokezana vijiti.BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger