Taasisi
mbalimbali zikiwemo za Serikali na binafsi kutoka ndani na nje ya nchi
zimeshiriki Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki, yanayofanyika
viwanja vya Rock City Mall Jijini Mwanza. Maonesho hayo huandaliwa na
Chama cha Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo nchini, TCCIA.
Taasisi
mbalimbali za Wajasiriamali, Wafanyabiashara na Viwanda hutumia
Maonesho hayo kukutana na wateja wapya, kutangaza na hata kuuza bidhaa
zake. Mbali na hilo taasisi mbalimbali hutumia fursa hiyo kukutana na
wananchi na kufikisha elimu husika.
Jeshi
la Polisi mkoani Mwanza kwa kujumuisha vitengo vyake ikiwemo Kikosi cha
Usalama barabarani na dawati la jinsia, limetumia maonesho hayo
kufikisha elimu mbalimbali kwa wananchi na hata kupokea maoni kutoka kwa
wananchi.
Na BMG
Banda la Jeshi la Polisi mkoani Mwanza, Kitengo cha dawati la jinsia
Banda la Jeshi la polisi mkoani Mwanza, kitengo cha Usalama barabarani
Maonesho
hayo yalianza Agosti 26,2016 na ufungi rasmi kufanyika Agosti 30,2016
ambapo Mkuu wa Wilaya ya Ilemela alifungua Maonesho hayo kwa niaba ya
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kama picha inavyoonekana mgeni rasmi akiwa kwenye
banda la jeshi la polisi mkoani Mwanza.
Endelea kutazama picha, Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza, akikagua mabanda ya washiriki mbalimbali
SHARE
No comments:
Post a Comment