TRA

TRA

Monday, November 14, 2016

Siku ya Kisukari Duniani- Muhimbili Yawapima Kisukari Wafanyakazi Wake

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


kik1
Dk Elias Mwandwani akimpima kisukari mmoja wa wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
kik2
Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru akiwa amevaa beji ikiwa ni ishara ya kuwamasisha wafanyakazi wa hospitali hiyo kupima kisukari.
kik3
Juma Selemani akipima uzito Leo kabla ya kupima kisukari  katika Hospitali hiyo.
kik4
Dk Faraja Chiwanga wa Muhimbili akimpima kisukari Juma Selemani katika hospitali hiyo.
Na Neema Mwangomo
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jana imeadhimisha siku ya kisukari duniani kwa kuwapima kisukari wafanyakazi wa hospitali hiyo.  
Jana wafanyakazi wa hospitali hiyo walikuwa wakipimwa kisukari na uzito pamoja na kupatiwa ushauri jinsi ya kupunguza uzito kwa wale waliobainika kuwa na uzito mkubwa.
Wafaanyakazi waliojitokeza  jana ni madaktari, wafanyakazi  kurugenzi za utawala, wauguzi na wanafanyakazi mbalimbali wa hospitali hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo Profesa Lawurence Museru alikuwa mstari wa mbele katika kuwashawishi wafanyakazi kupima kisukari. 
Naye Mkuu wa Kitengo cha Kisukari, Dk Mohamed J. Mohamed amesema Muhimbili imeona kuna umuhimu wa kupima kisukari kwa wafanyakazi wake kutokana na kubanwa na shughuli mbalimbali na hivyo mara nyingi wamekuwa wakikosa nafasi ya kupata huduma za afya.
“Tumeona ipo haja ya kutoa huduma hii kwani kuwa mfanyakazi wa Muhimbili haimaanishi kwamba upo salama kiafya hivyo tunafanya hivi ili wapate nafasi ya kupia kisukari,” amesema Dk Mohamed. (P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger