Mwenyekiti
wa TUGHE, Tawi la Muhimbili, Mziwanda Salumu Chimwege akimkabidhi
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa
Lawrence Museru zawadi kutoka kwa wahudumu wa hospitali.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili ( MNH), Profesa Lawrence
Museru leo amekutana na wahudumu wa Afya katika hospitali hiyo
pamoja na mambo mengine amewasisitiza kufanya kazi kwa bidii na kwamba
uongozi wa hospitali hiyo utaendelea kutatua changamoto
zinazowakabili.Pia, mkurugenzi huyo amewataka wahudumu hao kuzingatia
maadili ya kazi ili kutoa huduma bora kwa wagonjwa.
Profesa
Museru ametoa kauli hiyo jijini Dar es salaam katika mkutano na
baadhi ya wahudumu wa afya uliolenga kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo.
Profesa
Museru amesema licha ya wahudumu hao kukabiliwa changamoto mbalimbali ,
lakini hawanabudi kufanya kazi kwa bidii kwani jukumu lao ni kutoa
huduma bora.
"
Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayofanya hatua ambayo imesaidia kupunguza
malalamiko wakati wa kutoa huduma , ingawa bado kuna changamoto lakini
hatua budi kutoa huduma bora na sisi tutaendelea kutatua changamoto
hizo kadiri inavyowezekana ili kuhakikisha mazingira yetu ya kazi
yanakua bora," amesema Profesa Museru.
Katika
mkutano huo wahudumu hao wamewasilisha ajenda 14 ikiwamo ombi la
kupatiwa mafunzo ili kuongeza ufanisi na kuboresha utendaji kazi wao.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence
Museru akifafanua jambo kwenye mkutano huo. Kulia ni Mkurugenzi wa
Uuguzi, Agnes Mtawa wa hospitali hiyo.
Kaimu
Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji katika Hospitali ya Taifa Muhimbili
(MNH), Dk Mtemi Sufiani Baruani, Mkurugenzi wa Uuguzi, Agnes Mtawa,
Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru, Kaimu
Mkuu wa Idara ya Utawala, Leila Komba, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba
Shirikishi, Dk. Praxeda Ogweo na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba, Hedwiga
Swai wakiwasikiliza wahudumu wa hospitali hiyo katika mkutano
uliowahusisha viongozi hao. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa
jengo la maabara kuu.(P.T)
SHARE








No comments:
Post a Comment