TRA

TRA

Tuesday, February 28, 2017

Rais wa Somalia atangaza ''janga la kitaifa''

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Rais mpya wa Somalia, Mohamed Abdullahi Mohamed Farmajo leo ametangaza ''janga la kitaifa'' kutokana na ukame mkali ambao mashirika ya misaada yamesema umewaingiza kiasi ya watu milioni tatu katika mzozo. Rais Farmajo ameiomba jumuiya ya kimataifa kushughulikia haraka mzozo huo ili kuzisaidia familia na watu binafsi kutoka katika janga la ukame na kuepusha maafa ya kibinaadamu. Shirika la Afya Duniani, WHO jana lilionya kuwa Somalia iko katika hatari ya kukumbwa na njaa kwa mara ya tatu ndani ya kipindi cha miaka 25. Njaa ya mwaka 2011 iliwaua kiasi ya watu 260,000. Wakati huo huo, ukame umesababisha kuenea kwa magonjwa ya kuambukiza kama vile kuhara, kipindupindu na surua na karibu ya watu milioni 5.5 wako katika hatari ya kupatwa na magonjwa hayo.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger