TRA

TRA

Tuesday, February 28, 2017

Duterte aiomba radhi Ujerumani

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Rais wa Ufilipino, Rodrigo Duterte, ameiomba radhi Ujerumani kwa kushindwa kuzuia kuchinjwa kwa mateka wa Kijerumani aliyekuwa anashikiliwa na wanamgambo. Amesema operesheni kabambe ya ndege za kivita dhidi ya wanamgambo wenye itikadi kali inaendelea. Maafisa wa Ufilipino wamesema Jurgen Gustav Kantner aliuawa kwa kuchinjwa na wanagambo wa Abu Sayyaf kusini mwa Ufilipino baada ya muda uliowekwa kwa ajili ya kulipa fedha ili aweze kuachiwa huru kumalizika Jumapili. Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel amelaani vikali mauaji hayo akisema hicho ni kitendo cha kuchukiza. Duterte ameelezea jinsi serikali yake inavyoshughulikia wimbi la utekaji nyara unaofanywa na wanamgambo hao wenye itikadi kali za Kiislamu, ikiwemo ombi kwa China la kusaidia katika doria katika eneo la bahari ya kimataifa linalopakana na kusini mwa Ufilipino, Malaysia na Indonesia, ambako matukio ya uharamia na utekaji nyara yamekuwa yakifanyika.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger