Rais wa Marekani, Donald Trump amesema anataka kufanya ongezeko kubwa
katika bajeti ya ulinzi. Ikulu ya Marekani imesema Trump anataka
kuongeza matumizi katika jeshi la nchi hiyo kwa kiasi cha Dola bilioni
54. Trump amesema moja ya majukumu muhimu zaidi kwa serikali ya
shirikisho ni bajeti ya Marekani. Afisa wa bajeti wa Ikulu ya Marekani,
amesema Trump ambaye leo atalihutubia Bunge la Marekani kwa mara ya
kwanza, ataliomba bunge hilo kuongeza matumizi ya Wizara ya Ulinzi
katika mwaka ujao wa fedha kwa Dola bilioni 54, katika pendekezo lake la
kwanza la bajeti na kupunguza kiasi kama hicho kutoka kwenye matumizi
yasiyo ya ulinzi, ikiwemo kupunguza kwa kiasi kikubwa misaada kwa
mataifa ya kigeni. Hata hivyo, wabunge wa chama cha Democratic na
Republican ambao lazima waipitishe bajeti hiyo, wote wanalipinga
pendekezo hilo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment