Chemba
 ya biashara, viwanda na kilimo( TCCIA) inatarajia kufanya ziara ya 
kibiashara nchini Italy na Uturuki ambapo Chemba inapenda kuwakaribisha 
wafanyabiashara walio wanachama na wasio wanachama kuungana nasi kwenye 
mkutano huu wa wawekezaji. Chemba inawakumbusha kwamba, imabaki siku 
moja kwa wafanyabiashara wa Italy kuthibitisha ushiriki wao ambapo 
mwisho ni tarehe 3 March 2017. Kwa 3wafanyabiashara wa Uturuki wana muda
 mrefu ambapo muda wa mwisho wa kuthibitisha ushiriki wao ni tarehe 30 
March 2017. Ziara hii inatarajia kufanyika mwanzoni mwa mwezi May. 

Akizungumza
 na waandishi wa habari Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TCCIA Ndugu Gotfrid
 Muganda alisema “Lengo kubwa la ziara hii ni kuwawezesha 
wafanyabiashara wa Tanzania kutanua wigo wa masoko na fursa za 
kibiashara na kubadilishana ujuzi”. Akizungumza juu ya ziara hiyo 
Mkurugenzi wa EAG Group ambao ni washauri wa biashara na masoko wa TCCIA
 Imani Kajula alisema “Ukuzaji wa masoko ya nje ni mkakati endelevu 
ambao sio tu utaongeza soko nje lakini pia kuleta urari mzuri wa 
biashara na hivyo kusaidia kuimarisha thamani ya shilingi”. Aliwaambia 
wafanyabiashara ambao ni wanachama na wasio wanachama wanakaribishwa 
kijiandikisha ambapo mwisho kwa wanaoenda Italy ni tarehe 3 March 
2017..
  SHARE 
  
 
 









 
No comments:
Post a Comment