TRA

TRA

Saturday, April 15, 2017

Syria, Iran ana Urusi wameionya Marekani

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

 
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Syria, Iran na Urusi wameionya Marekani dhidi ya mashambulizi yake kwa Syria katika mkutano wao uliofanyika mjini Moscow Urusi. 
 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergey Lavrov, pamoja na wenzake wa Iran na Syria wamelishitumu vikali shambulizi la anga la hivi karibuni lililofanywa na Marekani katika kambi ya kikosi cha anga cha Syria.
 
 
 
                          Bashar Assad

 Lavrov amesema hatua yoyote nyingine kama hiyo itakayochukuliwa na Marekani itakuwa na athari kubwa kwa usalama wa dunia. 
 
Hata hivyo wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema taifa hilo halijafanya uamuzi wowote mwingine wa kufanya mashambulizi zaidi. 
 
Msemaji wa wizara hiyo Mark Toner amesema Urusi ingetumia ushawishi wake kwa Assad kuhakikisha vita katika taifa hilo la Mashariki ya Kati vinamalizika kabisa.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger