TRA

TRA

Monday, May 29, 2017

Huddersfield Town wapandishwa daraja kucheza EPL

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

 Huddersfield walimaliza nafasi ya tano katika ligi ya Championship 

Klabu ya Huddersfield Town imepandishwa daraja kucheza Ligi ya Premia kwa mara ya kwanza baada ya kulaza Reading 4-3 kupitia mikwaju ya penalti uwanjani Wembley Jumatatu.

Baada ya kutoka sare 0-0 dakika 120, Town walitakiwa kupiga mikwaju kwa mara ya pili na walikuwa na bahati tena baada ya kulaza pia Sheffield Wednesday kwa mikwaju ya penalti hatua ya nusufainali.

 Reading walimaliza nafasi ya tatu kwenye jedwali ligi ya Championship, alama nne juu ya Huddersfield

Christopher Schindler aliwashindia Town baada ya mkwaju wa Liam Moore kupaa angani nao mpira wa Jordan Obita ukaokolewa na kipa Danny Ward.


Klabu hiyo ya Yorkshire Magharibi haijacheza soka ya ligi kuu tangu 1972.

Reading, waliomaliza alama nne na nafasi mbili juu ya Town waliokuwa nafasi ya tano katika ligi ya Championship sasa wameshindwa katika fainali ya muondoano ya kufuzu kwa EPL baada ya ligi kwa mara ya nne.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger