Kiongozi mkuu wa
upinzani nchini Venezuela Henrique Capriles amesema alipokonywa hati
yake ya kusafiria uwanja wa ndege alipokuwa akijiandaa kwenda New York.
Capriles pia anahudumu kama gavana wa jimbo la Miranda
Capriles amekuwa muhimili wa kuchochea maandamano yanayoendelea nchini Venezuela.
Miezi miwili iliyopita alifungiwa kushiriki kwenye siasa kwa miaka 15 kwa tuhuma za kuleta uchochezi.
Katibu mkuu wa jumuiya ya nchi za Amerika Luis Almagro amesema kitendo hicho ni ukiukwaji wa haki za binaadamu.
CHANZO; BBC
SHARE









No comments:
Post a Comment