TRA

TRA

Monday, May 15, 2017

MSHAMBULIAJI WA MAMELOD SUNDOWNS ATUA SINGIDA UNITED

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


IMG-20170514-WA0036[1]
Singida United imedhamiria kuleta mapinduzi ya soka hapa nchini baada ya klabu hiyo kuendelea kujiimarisha zaidi kwenye usajili wa wachezaji.
Baada ya kufanikiwa kusajili wachezaji wanne wa kigeni leo hii uongozi wa klabu hiyo umekamilisha usajili wa mshambuliaji aliyewai kuitumikia ya Mamelod Sondowns na Super Sport za nchini Afrika ya Kusini.
Mshambuliaji huyo anaetambulika kwa jina la Nhivi Simbarashe anakuwa mchezaji wa tano kusajili ndani ya klabu hiyo itakayoongozwa na kocha mahili Hans van Der Pluijm na msaidizi wake Fredrick Minziro.
Simbarashe pia ni mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Zimbabwe amekuwa na mafanikio makubwa kwenye timu alizochezea ikiwemo kufunga goli pekee ambalo liliwaondosha TP Mazembe katika ushiriki wa michuano ya kombe la klabu bingwa barani Afrika wakati akiitumikia timu ya Mamelod Sondowns.
Uongozi wa Singida United umethibitisha kumpa kandarasi ya miaka miwili mchezaji huyo akitokea klabu ya Caps United ya nchini Zimbabwe ambapo baada ya kutokea Afrika Kusini alijiunga na timu hiyo ya nchini kwake.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger