TRA

TRA

Monday, May 29, 2017

SERIKALI YAONGEZA MASHINE 4 KWAAJILI YA KUDHIBITI UGONJWA WA EBOLA MIPAKANI.

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


unnamed
Waziri wa Afya ,Maendeleo yajamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiongea mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kujikinga na Ugonjwa wa Ebola  uliopo nchini Congo ili usiingie Tanzania.
…………………………
Na Ally Daud-WAMJW DAR ES SALAAM
SERIKALI imeongeza mashine nne za kupimia virusi vya ugonjwa wa Ebola katika mipaka ya Holoholo,Mutukula,Rusumo na Silali ili kudhibiti na kutambua hali ya maambukizi ya ugonjwa huo kwa wasafiri wa ndani na nje ya Tanzania.
Akizungumza hayo wakati wa mkutano na waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa hatua mbalimbali zinachukuliwa kuhusu kujikinga na ugonjwa huo usiingie nchini.
“Moja ya hatua tuliyochukua kama Wizara ya Afya ni kuweka mfumo wa kufuatilia magonjwa (Intergreted Disease available system) na kujua  taarifa za wasafiri katika mipaka yote kwa  wanaotoka nchini Congo kuingia Tanzania ili kujua wanapotoka mpaka wanapofikia hakuna maambukizi ya ebola “ alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa mbali na hatua hizo Serikali imegawa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Ebola ikiwemo gauni la kujikinga,mawani,mabuti pamoja na vidonge vya Chroline katika mipaka yote ili kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo kwa watumishi wanaofanya kazi mipakani.
Kwa mujibu wa Waziri Ummy amesema kuwa wanaendelea kutoa elimu kwa kuweka mabango yanayohusu ebola katika mipaka yote na vituo vya kusafiria ikiwemo viwanja vya Ndege,Bandari na vituo vya mipakani na kupitia njia ya simu kwa kupiga namba 117 kwa mitandao yote.
“Hakuna mtu aliyethibitishwa kuwa na ugonjwa wa ebola nchini Tanzania hivyo watanzania msiwe na hofu ila tuchukue tahadhari na kupata elimu zaidi ili kujikinga na ugonjwa huu” alisisitiza Waziri Ummy.
Mbali na hayo Waziri Ummy ameamua kuunda timu huru ya watu sita itakayoongozwa na Daktari Bingwa wa magonjwa ya kinamama Prof. Charles Majige ili kuchunguza upya tukio la Bi. Asma Elias ya kuibiwa kichanga  katika hospitali ya Temeke baada ya kukataliwa ripoti ya awali iliyotolewa na Mganga Mkuu wa Dar es salaam.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger