TRA

TRA

Monday, May 29, 2017

DARUSO Yampongeza JPM Kwa Kusimamia Rasilimali za Taifa

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


1
Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO) akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa Habari uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam ukilenga kutoa tamko la DARUSO kuhusu kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali hasa matokeo ya Tume ya kuchunguza kiwango cha madini kwenye makontena 277.Kulia ni Waziri wa Ulinzi wa Serikali hiyo Bw. Richard Augustine na kushoto ni Waziri Mkuu wa Serikali hiyo Bw. Sintau Fredrick
unnamed
 Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO) akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa Habari uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam .
(Picha  na Frank Mvungi-Maelezo)
…………………
Frank Mvungi-MAELEZO
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amepongezwa na Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (DARUSO) kwa kusimamia vyema rasilimali za Taifa ili ziweze kuwanufaisha watanzania wote.
Kauli hiyo  imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na  Rais wa (DARUSO) Bw.John Jilili wakati wa mkutano wao na vyombo vya habari uliolenga kutoa tamko la kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais kwa kuunda Tume iliyochunguza na kutoa matokeo kuhusu mchanga (makinikia) unaosafirishwa nje ya nchi.
“Kuanzia  sasa uchakataji (processing) ufanyike hapa nchini na mikataba yote iwe na kipengele kinachoyalazimisha makampuni yanayopewa leseni ya kuchimba madini kuwa na mitambo ya kuchenjua makinikia ya madini yanayozalishwa na migodi hiyo.” alisema  Jilili
Akifafanua zaidi Jilili amesema kuwa mikataba yote ya Madini ni vyema ikatazamwa upya na kuzingatia maslahi mapana ya Taifa na si ya watu wachache, kwani kwa kufanya hivyo kuonyesha dhamira ya dhati ya Serikali katika kuleta mageuzi katika sekta ya madini nchini.
Katika mapendekezo yao DARUSO imebainisha kuwa Watanzania wangependa kuona Mikataba na Sheria zilizopo zinaruhusu ukaguzi wa mara kwa mara migodini ili Serikali ijiridhishe kuhusu kiwango cha madini kinachozalishwa katika migodi hiyo pamoja na Serikali kuwa na ubia wa asilimia 50 au 49 na wawekezaji katika sekta ya madini.
Aidha Jilili alisema vyema pia kwa vyema kwa Viongozi wote waliopewa dhamana ya kuwaletea wananchi maendeleo wakatekeleza wajibu huo kwa uzalendo na kuepuka kuingia mikataba inayowezesha kuiletea hasara Serikali.
“Tunapenda kuwaomba watanzania wote wasomi na wasio wasomi kumsaidia Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kufikia lengo lake la kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi na hayo yanawezekana tu kwa kuweka uzalendo mbele na maslahi ya Taifa kwanza.” Alisisitiza Jilili
Aliongeza kuwa nidhamu na uwajibikaji katika sehemu za kazi ni jambo la muhimu kwa Watendaji waliokabidhiwa majukumu ya kusimamia sekta mbalimbali kwani kwa kufanya hivyo  kutawezesha kuzaliwa kwa Tanzania mpya chini ya Uongozi wa Serikali ya awamu ya Tano.
“DARUSO inamthibitishia Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Watanzania wote kuwa iko sambamba nae katika harakati zake za kuikomboa nchi yetu katika Nyanja zote ikemo kiuchumi” Alisisitiza Jilili

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger