Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Biashara Afrika Tawi la
Tanzania (CBA Tanzania), Gift Shoko akizungumza na baadhi ya wateja
wakubwa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, wakati
benki hiyo ilipoandaa futari mahsusi. Kati ya mengi aliyoeleza, Shoko
aliwahakikishia wateja wa benki hiyo jitihada madhubuti na endelevu
zinazoendelea kufanya na benki ya CBA kwa kuboresha huduma na bidhaa
zake wakati wote. Hafla hiyo ilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara ya
Afya, Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk.
Hamis Kigwangala kama mgeni rasmi.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza
alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Benki ya
Biashara Afrika Tawi la Tanzania (CBA Tanzania), Jijini Dar es Salaam.
Wateja wakubwa wa Benki ya
Biashara Afrika Tawi la Tanzania (CBA Tanzania), wakipakua futari
iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki
iliyopita.
Mkuu wa Masoko wa Benki ya CBA
Tanzania, Solomono Kawiche (wa kwanza kulia) akimuongoza na Naibu Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Hamisi
Kigwangalla pamoja na Mke wake kupakua futari.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Biashara Afrika Tawi la
Tanzania (CBA Tanzania), Gift Shoko (wa kwanza kushoto) akipakua futari
pamoja na wateja.
Wateja wakipata futari kwa pamoja.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Biashara Afrika Tawi la Tanzania (CBA Tanzania), Gift Shoko (kulia) akibadilishana mawazo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamisi Kigwangalla pamoja na mteja wa CBA Benki.
SHARE
No comments:
Post a Comment