TRA

TRA

Friday, June 23, 2017

Dkt. Pallangyo akutana na Watendaji kutoka Benki ya Dunia

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 
Na Rhoda James Leo Juni 23, 2017 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo amekutana na Watendaji kutoka Benki ya Dunia (WB) waliomtembelea kwa ajili ya kupata taarifa ya maendeleo ya miradi mbalimbali ya madini inayotekelezwa na Wizara. Kati ya masuala yaliyojadiliwa ni pamoja na uimarishaji wa Sekta ya Madini, Mafanikio ya miradi yake pamoja na taasisi.
MWASE1
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Juliana Pallangyo (mbele) akielezea miradi ya Sekta ya Madini na mafanikio yake. Wengine katika Picha ni Ujumbe kutoka Benki ya Dunia (WB), Viongozi Waandamizi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).
MWASE2
Watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wakiwa katika kikao hicho.
MWASE3
Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia Sudeshna Banerjee ( wa kwanza kulia) akielezea mipango walionayo katika kusaidia utekelezaji wa Miradi ya Sekta ya Madini ili iendane na Vipaumbele vya Serikali.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger