TRA

TRA

Friday, June 23, 2017

OFISI YA WAZIRI MKUU YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


unnamed
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua akiongea na  wafanyakazi wa ofisi hiyo (hawako pichani) wakati wa mkutano wa kuadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma uliofanyika    leo jijini Dar es salaam tarehe 23 Juni, 2017.
1
Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mjadala wakati wa mkutano wa Kuadhinmisha wiki ya utumishi wa umma uliofanyika    leo jijini Dar es salaam tarehe 23 Juni, 2017.
2
Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mjadala wakati wa mkutano wa Kuadhinmisha wiki ya utumishi wa umma uliofanyika    leo jijini Dar es salaam tarehe 23 Juni, 2017.
3
Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mjadala wakati wa mkutano wa Kuadhinmisha wiki ya utumishi wa umma uliofanyika    leo jijini Dar es salaam tarehe 23 Juni, 2017.
4
Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mjadala wakati wa mkutano wa Kuadhinmisha wiki ya utumishi wa umma uliofanyika    leo jijini Dar es salaam tarehe 23 Juni, 2017.
…………………….

Ofisi ya Waziri Mkuu imeadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma ambayo hufanyika kila mwaka kuanzia Juni 16-23 Barani Afrika,  kwa mwaka huu kauli mbiu  ni “Kuimarisha Ushirikishwaji wa Jamii katika Utoaji Huduma: Vijana washirikishwe kuleta Mabadiliko Barani Afrika”.
Kwa kuzingatia kauli mbiu hiyo yenye kujikita katika kushirikisha jamii katika utoaji huduma, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua amekutana na wafanyakazi wa ofisi hiyo leo jijini Dar es salaam tarehe 23 Juni, 2017,   ambapo wamejadili jinsi ya kuboresha utoaji wa huduma kwa umma kwa kuzingatia weledi, uadilifu na ufanisi ili kuhakikisha Dira na Dhima ya Ofisi hiyo inafikiwa.
Dira ya Ofisi hiyo ni kutoa huduma kwa umma katika mazingira shindani ya kiuchumi ili kuwa na maendeleo emdelevu, aidha Dhima ya ofisi hiyo ni Kuratibu na kusimamia utoaji wa huduma zenye kuleta matokeo yanaotarajiwa katika sekta zote ili kujenga mazingira ya kiuchumi kwa maendeleo enndelevu.Ofisi ya Waziri imekuwepo tangu mwaka 1962. Mwaka 1977, Ofisi ilipewa hadhi yake kisheria kwa kuzingatia Katiba ya  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ilianzisha wadhifa wa Waziri mkuu.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger