Naibu Mkurugenzi wa Halotel, Nguyen Van Son akiweka laini ya simu ya Halotel kwa mteja mpya wa mtandao huo, Salim Selemani, ambaye amejiunga na wakati wa uzinduzi wa kampeni ya “Switch to Halotel” yenye lengo la kuwahamasisha Watanzania kujiunga na mtandao huo. Kampeni hiyo pia itahusisha wafanyakazi wa halotel kutembelea maeneo mbalimbali na kutoa huduma kwa wateja katika maeneo yao. Pamoja naye katika picha ni Meneja Miradi wa Kampuni hiyo, Frank Mwakyoma na waendesha pikipiki wa kituo cha Makumbusho.
Kampuni ya mawasiliano ya simu ya Halotel, imezindua kampeni mpya ya Switch to
Halotel, yenye lengo la kuwahamasisha Watanzania kujiunga na Mtandao huo
sambamba na kuzindua utaratibu wa wafanyakazi wa kampuni hiyo kuwatembelea
wateja wa Mtandao huo katika maeneo yote nchi nzima mjini na vijijini.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo iliyofanyika katika soko la Makumbusho
lililoko Kinondoni Dar es Salaam, Naibu Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Nguyen
Van Son, amesema tangu kuzinduliwa kwa huduma za kampuni hiyo, wamepata
mapokezi mazuri kutoka kwa watanzania ambao hadi sasa zaidi ya wateja milioni
tatu na laki tano, tayari wamejiunga na mtandao huo na wanafurahia huduma mbalimbali
zinazotolewa na kampuni hiyo ya simu.
“Tunafarijika
sana kwa namna ambavyo Watanzania wameendelea kutuunga mkono katika jitihada
zetu za kuboresha huduma za mawasiliano kwa jamii hii, ni faraja kubwa kwetu
kwamba katika kipindi hiki kifupi tumepata mafanikio makubwa na bado
tunaendelea kupata wateja wanaojiunga na mtandao wetu siku hadi siku,” Jambo
hili linatufanya tusilale tufikilie ni namna gani tunapaswa kuendelea kukizi
mahitaji yao.
“Kuzinduliwa
kwa kampeni hii itakuwa ni sehemu ya sisi kusogea karibu na wateja wetu,
kuwahudumia pamoja na kuwasikiliza ni nini wanahitaji kutoka kwetu,” Tunaamini
kabisa kwamba kuwa karibu na wateja wetu tutajenga mtandao bora kabisa utakao
kuwa na huduma zinazolenga maisha halisi ya Watanzania.
Aidha
Naibu Mkurugenzi huyo alitaarifu kuwa, Kampuni hiyo imeanza utaratibu wa kuwa
na vifurushi Maalumu kulingana na maeneo na mahitaji ya wateja husika, Huku
akitolea mfano wa kuwa na vifurushi maalumu kwa wateja wa Mtandao huo wa
Zanzibar ambao wameanzishiwa kifurushi maalumu cha ZANZIBAR YETU, ambacho kwa
watumiaji wa Halotel wataweza kuongea bure siku za mwisho wa wiki kwa shilingi
1000 pamoja na vifurushi vingine, Kwa wateja wapya wa mikoa ya Mbeya, Manyara,
Pwani, Arusha, Kilimanjaro na Mara, Mkoa huo wanaweza kupata dakika 60 za
kupiga simu bure ndani ya mtandao kila wanapoweka muda wa maongezi kwa siku 30
baada ya kusajili . Pamoja na Ofa ya Kiboko yao ambayo inapatika katika baadhi
ya minara ya 3G ya mtandao huo.
Naibu
Mkurugenzi huyo alibainisha kuwa, licha ya kuboresha na kutoa huduma
zinazowalenga Watanzania, kampuni hiyo pia imeendelea kufanya uwekezaji mkubwa
katika kuboresha Mawasiliano na ubora wa Mtandao huo ambapo hivi karibuni
mtandao huo ulitangaza uwekezaji wa zaidi ya bilioni 200 kwa ajiri ya kuboresha
ubora wa sauti na kasi ya intaneti, huku wakitarajia kuwekeza zaidi katika
mwaka ujao wa fedha.
SHARE
No comments:
Post a Comment