TRA

TRA

Friday, June 30, 2017

HANS POPPE: KWELI NIMEHOJIWA NA TAKUKURU

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amesema alihojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Hans Poppe amesema alihojiwa lakini akaachiwa na si anashikiliwa kama ambavyo imekuwa ikielezwa.

“Nilikwenda, nikahojiwa na baadaye nimeondoka, niko mitaani. Si kweli kwamba ninashikiliwa.

“Kuhusiana na kuhojiwa tayari nilihojiwa kama mara mbili hivi kabla. Haya ni mambo yanatokea,” alisema Hans Poppe.

Jana kulikuwa na taarifa kwamba Hans Poppe naye alikuwa anashikiliwa na Takukuru baada ya Rais wa Simba, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ kupandishwa kizimbani.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger