Naibu waziri wa ardhi nyumba na
maendeleo ya makazi Angelina mabula akizungumza na watumishi wa
halmashauri za Mji na Wilaya ya musoma mkoa wa Mara.
……………
Na Mwandishi Maalum – Musoma
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na
Maendeleo ya Mkazi Angelina Mabula amesema ni marufuku halmashauri
kuchukua maeneo ya wananchi bila ya kuwalipa fidia.
Mhe. Mabula amesema hayo Wilayani
Butiama mkoa Mara wakati wa ziara yake yenye nia ya kutatua migogoro ya
ardhi pamoja na kukagua mfumo wa ukusanyaji kodi ya ardhi.
Amesema wakati wa mchakato wa
kuchukua maeneo ya mwananchi ni vyema wahusika wakashirikishwa kuanzia
hatua ya awali sambambana na kuelimishwa juu ya zoezi hilo ili kuepuka
migogoro inayoweza kutokea.
‘’cha msingi ni kuanza kuzungumza
na mwananchi kabla ya kuchukua eneo lake na kumueleza eneo ambalo
ataachiwa na halmashauri zihakikishe mwananchi huyo anapimiwa pamoja na
kupatiwa hati yake’’ alisema Mabula
Aidha, mhe. Mabula amesema eneo
litakalochukuliwa na halmashauri viwanja vyake kuuzwa fedha
itakayopatikana halmashauri ihakikishe inatumika katika kutengeneza
miundo mbinu na huduma nyingine za jamii na kusisitiza kuwa kwa kufanya
hivyo migogoro haiwezi kutokea.
Naibu waziri wa ardhi nyumba na
maendeleo ya makazi ameziagiza halmashauri kuhakikisha zinapanga miji
kulingana na ‘master plan’ ili kuwa miji bora iliyopangika
SHARE
No comments:
Post a Comment